Search This Blog

Friday, January 13, 2012

VILLAS BOAS: LAMPARD AUZWI, BADO NAMUHITAJI.


Frank Lampard ameambiwa kwamba anabakia kuwa mchezaji muhimu katika mipango ya Chelsea hata kama kwa sasa sio mchezaji anayeanza kila siku.

Future ya Lamapard imekuwa ikizua gumzo tangu Andre Villas Boas alipoanza kumueka benchi.

Sportmail liliripoti wiki iliyopita kwamba Manchester United walikuwa wakijipanga kutake advantage ya hali hiyo katika kocha na kiungo huyo ili wapeleke ofa ya kumsajili.

Lakini Villas-Boas amesema Lampard, 33, anakubaliana na majukumu anayopewa ndani ya klabu hiyo.

Mreno huyo alisema: “Kwa hakika, Lampard hauzwi. Kila mchezaji anataka kupata nafasi ya kucheza.

“Ni kawaida kila mchezaji anataka kuhusika katika upangwaji kikosini. Frank, na jinsi alivyo na historia anayoiwakilisha, anataka kucheza muda wote, lakini kila mchezaji anashindania nafasi.

“Nimeshasema msimu hivi msimu mzima, hata kama Frank atakuwa akipata uda wa kucheza kuliko wengine, na ukiangalia kwa umakini Frank ni mchezaji wa tano au sita katika wale wanaongoza kutumika at Chelsea.”

Wakati huo huo, Chelsea wamekataa ofa ya £3million kutoka Queens Park Rangers kwa ajili ya mlinzi Alex.

Villas Boas ana matumaini ya kumsaini rasmi Gary Cahil kutoka Bolton mapema kabla ya mchezo dhidi ya Sunderland.

No comments:

Post a Comment