Search This Blog

Friday, January 13, 2012

SILVA ATOA ONYO: MECHI ZOTE ZIJAZO TUTACHEZA KAMA FAINALI


David Silva jana usiku alitoa onyo kwa wapinzani wao na kuwaambia wachezaji wenzake wa Manchester City : Tuchezeni mechi zote zilizobakia kama fainali.”

Mhispania huyo ambaye kwasasa anajiuguuza na maumivu ya kifundo cha mguu alikuwa jukwaani akiangalia namna timu yake ikipoteza mechi yake ya pili katika uwanja wao dhidi ya Liverpool ndani ya kipindi cha masaa 72.

Silva sasa anajipanga kucheza dhidi ya Wigan Jumatatu, huku City wakiwa wanajipanga kuongeza wigo wa pointi katika uongozi wao wa premier league, na kuwaacha Spurs na United wakigombea nafasi ya pili.

“Kutolewa katika FA Cup na United ilikuwa uchungu sana – tulikuwa tunataka sana kurudisha ubingwa ule.

Lakini iliniuma zaidi kuona timu yangu ikifungwa katika Carling nikiwa naangalia jukwaani. Yalikuwa matokeo mabaya na naamini tutaibuka katika mchezo wa pili @Anfield. Bado tuna nafasi nzuri ya kufika fainali.” Alimaliza Silva.

No comments:

Post a Comment