Search This Blog

Friday, October 7, 2011

KOCHA MOSES BASENA KUMPA SOMO BOBAN

Kocha wa klabu ya Simba Mganda Moses Basena amesema kuwa anatambua matatizo ya mchezaji Haruna Moshi Boban na sasa anajipanga vizuri ili kuweza kuyashughulikia kwa faida ya timu yake kufanya vizuri katika mashindano inayoshiriki.

Kauli hii ya Basena inakuja siku moja tangu zitoke taarifa kuwa uongozi wa klabu hiyo unajipanga kumfungia boban na wenzie ambao ni wategaji wa mazoezi katika klabu hiyo.

Akizungumza na blog hii Basena alisema “"Nitakaa na Boban niongee naye, nitaendelea kumshawishi apende mazoezi, Boban namkubali ni mchezaji mzuri, lakini huwezi kuwa mzuri uwanjani halafu mazoezi ukazembea, ni lazima afuate programu yangu,"alisema.

No comments:

Post a Comment