Search This Blog

Thursday, October 6, 2011

BOBAN, YONDANI, OKWI NA MWAKINGWE HATARINI KUFUNGIWA SIMBA

Taarifa ambazo hazijathibitishwa na uongozi wa klabu ya Simba zinasema kuwa wachezaji Haruna Moshi ‘Boban’, Kelvin Yondani, Emmanuel Okwi na Ulimboka Mwakingwe wapo katika hatari ya kufungiwa ama kusimamishwa na klabu hiyo kutokana utovu wa nidhamu.

Taarifa kutoka moja ya chanzo cha habari kilicho karibu na uongozi wa timu hiyo kinasema kuwa wachezaji hao wote wana makosa yanayofanana ya kutofika mazoezini huku wengine wakitoa sababu zisizo za kweli na wengine wakiwa kimya tu, wanatarajiwa kujadiliwa na uongozi wa timu pamoja na benchi la ufundi la timu hiyo kabla ya maamuzi ya kuwapa adhabu kali kutolewa.

No comments:

Post a Comment