Search This Blog

Thursday, October 6, 2011

VICTOR COSTA AACHWA STARS-CANNAVARO ACHUKUA NAFASI YAKE


Beki wa kutumainiwa wa klabu ya Simba Victor Costa “Nyumba” ameachwa katika kikosi cha timu a Taifa baada ya kupata maumivu ya nyonga.

Kutokana na Costa kuumia kocha Jan Poulsen jana alimuita kikosini beki wa Yanga Nadir Haroub Cannavaro kwa ajili ya kuziba nafasi iliyoachwa na Costa.

Taifa Stars imeondoka leo kuelea Morocco kwa ajili ya mechi ya mwisho ya kundi linalozihusisha timu za Algeria, Morocco, Afrika ya Kati na Tanzania katika kugombania nafasi ya kushiriki mashindano ya Kombe la mataifa huru ya Afrika litakalofanyika mwakani nchini Gabon na Equatorial Guinea.

No comments:

Post a Comment