Search This Blog

Friday, September 23, 2011

YANGA WAIWEKEA NGUMU TFF


Uongozi wa mabingwa wa Tanzania Bara Yanga SC, imepinga mabadiliko ya ratiba ya ligi kuu ya Tanzania Bara, kwa mchezo wao kusogezwa mbele mpaka jumatano badala ya jumamosi hii.

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania, TFF limesogeza mbele mchezo wa Yanga na Coastal Union mpaka september ya 28 siku ya jumatano, badala ya siku ya jumamosi september 24 mwaka huu.

Yanga wamepinga mabadiliko hayo ya ratiba kwa kusema kitendo cha kubadilisha ratiba ovyo ovyo kwa sasa hautumiki, huku wakitumia kielelezo cha TFF kukataa kuwasogezea mchezo baina yake na Kagera sugar msimu uliopita kutokana na wao kuwa na mchezo wa kimataifa.

Hata hivyo walisema kuwa hakuna haja ya kusogeza mchezo mbele wakati kuna uwanja wa Azam unaweza kupokea mchezo huo badala ya Taifa kama uwanja unavyo onyeshwa.

No comments:

Post a Comment