Search This Blog

Saturday, September 17, 2011

MTIHANI WA KWANZA KWA ANDRE VILLAS-BOAS

Kocha Andre Villas-Boas anakutana na mtihani wa kwanza mgumu akiwa kocha kesho jumapili, na nafikiri tutaona na kujua mengi kuhusu falsafa zake kwenye soka.

Chelsea hawajafungwa tangu mreno huyo mwenye miaka 33 alipowasili Stamford Bridge akitokea Porto.

Na nafikiri trip ya Chelsea kwenda Old Trafford itatuthibitishia ubora wa mbinu za Villas Boas.

Tunafahamu nini tutegemee kutoka kwa Manchester united ambao hawajawahi kucheza defensively dhidi ya timu yoyote iwe Barcelona au Wigan.

United hawatobadilisha mchezo wao dhidi ya Chelsea lakini kitachokuwa kinavutiwa zaidi ni kuona jinsi gani wageni watakavyocheza.

Vilas-Boas alipokuwa Porto alikuwa akitegemea kushinda kila mchezo lakini sasa yupo katika sehemu nyingine.

Anai-manage timu kubwa ambayo kesho inasafiri kwenda Theatre of Dreams ambako mwaka huu timu yao ipo katika form nzuri.

Hivyo nafikiri mchezo utatueleza na kutufanya kumjua vizuri Villas-Boas.

Je atafahamu kuwa ni vigumu sana kucheza na United kwa open game?

Au anaweza kwenda na akacheza aina ya mchezo huo na akafanikiwa.?

Nafahamu nini Jose Mourinho ambaye siku zote amekuwa akifananishwa na Villas-Boas-angeenda kufanya kama bado angekuwa kocha wa Chelsea.

Kama Mourinho angekutana na United ambayo ipo kwenye form nzuri, basi ni dhahiri angecheza mchezo wa kuzuia zaidi.

Hivyo natamani kuona je Villas Boas atacheza mtingdo wa 4-3-3 au 4-5-1 au 4-4-2 @ old Trafford.

Kesho naamini AVB atachagua kikosi chake bora kabisa kwa mara ya kwanza kitu ambacho tena kitakuwa cha kutazamwa ili kujua his assessment of his squad.

Haijalishi matokeo ya kesho, nina uhakika AVB atakuwa manager mzuri sana.

No comments:

Post a Comment