Search This Blog

Thursday, August 4, 2011

CANTONA: SNEIJDER NI ERIC MPYA


Manchester United icon Eric Cantona amemsisitiza Sir Alex Ferguson kumleta Wesley Sneijder Old Trafford huku amkisifia kiungo huyo wa Inter Milan kwa kusema, “Sneijder ni Eric Cantona mpya”.

Mfaransa huyo ambaye kwa sasa ni mkurugenzi wa soka katika klabu ya New York Cosmos, yupo jijini Manchester kushiriki katika mechi ya kumuaga Paul Scholes kesho Ijumaa, na sasa anaungana na Scholes ambaye juzi alimsifia Sneijder kama mchezaji sahihi kumrithi kutokana na mchezo wake wenye akili na maarifa.King Eric alikaririwa akisema: “Sneijder ni mtu ambaye Manchester United inahitaji.Hakuna mchezaji kama yeye kwa sasa, ana nguvu, muda mwingine ananikumbusha kuhusu Eric wa zamani.”

No comments:

Post a Comment