Search This Blog

Tuesday, July 26, 2011

SPURS WATAKA £9Mm KWA AJILI YA CROUCH


Tottenham wameweka bei ya kumnunua Peter Crouch kwa timu zinazomtaka kuwa £9million.

Newcastle wameonekana kuongoza mbio za kuisaka saini ya Crouch na Harry Redknapp amesema anataka kupata fedha aliyotoa kumnunua kutoka Portsmouth miaka miwili iliyopita.

Kiasi hicho cha pesa kinaonekana ni kizingiti kikubwa kwa watoto wa Mike Ashley ambao hawapo tayari kulipa fedha hiyo kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30.

Sunderland ambao wamekuwa wakimtamani Crouch kwa muda sasa, na walikuwa tayari kumbadilisha na Asamoah Gyan earlier this summer, lakini sasa Steve Bruce akiwa tayari amempata wonderkid Connor Wickham, Black Cats wanaonekana kubadili mawazo juu ya Crouch.

No comments:

Post a Comment