Search This Blog

Monday, July 25, 2011

EL CLASSICO KWENYE TUZO YA MCHEZAJI BORA ULAYA

Upinzani baina ya Real Madrid na Barcelona maarufu kama “El Classico” umeamia kwenye tuzo za mchezaji bora barani ulaya baada ya Cristiano Ronaldo, Lionel Messi na Xavi Hernandez kuchaguliwa kugombea tuzo hiyo.

Tuzo hizo zimepangwa kufanyika mwezi ujao baada ya wachezaji hao watatu kuchaguliwa na waandishi wa michezo 53 kutoka katika kila mwananchama wa UEFA katika listi ambayo pia imewahusisha Wayne Rooney na Andres Iniesta.

Kura za kuchagua mchezaji bora atakayeshinda tuzo hiyo zitapigwa August 25.

No comments:

Post a Comment