Search This Blog

Thursday, July 28, 2011

SAMBA: NIACHENI NIJIUNGE NA ARSENAL


Chris Samba ameiomba klabu yake ya Blackburn: Niacheni nijiunge na Arsenal.

Nahodha huyo alisema: “Nataka kucheza kwenye ligi ya mabingwa.Mchezaji asiyeota kuhusu hili.”

Beki huyu mfaransa, 27, alisaini mkataba mpya wa miaka 5 ya kuitumikia klabu hiyo ya Ewood Park miezi michache iliyopita, lakini amesisitiza: “Mchezaji ambaye ana uchu wa kucheza katika ngazi za juu basi atakuwa amekosea na amechagua mhezo usiomfaa.”

“Sijui nini wanachofanya Arsenal kwa sababu sishughuliki na na mambo hayo, hivyo hilo sio tatizo langu.

“Kwa sasa mimi bado mchezaji wa Blackburn lakini nitakuwa muongo mkubwa nikisema kila kitu kipo sawa na sitaki kucheza kwenye champions league.”

Arsene Wenger amekuwa akimfuatilia Samba mwenye thamani inayokadiriwa kufikia £12million lakini mpaka sasa ameshindwa kukamilisha dili hilo.

No comments:

Post a Comment