Search This Blog

Thursday, July 28, 2011

KUN AGUERO MCHEZAJI GHALI ZAIDI NDANI YA JIJI LA MANCHESTER


Sergio Aguero amemalizana na matajiri wa Manchester City hivyo kutangazwa kuwa mchezaji rasmi wa kikosi cha Roberto Mancini.

City wamekubali kulipa £38 kwa Atletico Madrid kwa ajili mkwe wa Diego Maradona, ambaye amesaini mkataba wa miaka 5 huku akiwa anapata mshahara wa £200,000 kwa wiki, hivyo kufanya thamani ya jumla ya uhamisho wake kuwa zaidi ya £85million.

Uhamisho huu wenye thamani £85m wa Aguero, 23, ambaye atavaa jezi no.16 ndio wa ghali zaidi katika historia ya vilabu vya jiji la Manchester.

No comments:

Post a Comment