Search This Blog

Wednesday, July 27, 2011

AGUERO ATUA ENGLAND KUMALIZANA NA CITY


Sergio Aguero ametua jijini Manchester kukamilisha uhamisho wake kutoka Atletico Madrid kwenda Eastlands kwa dili lenye thamani ya £38million.

Muargentina huyo alisafiri kutoka kwao jana Jumanne usiku mara baada ya klabu mbili kumalizana, na alitumia mtandao wa Twitter kuelezea kuwasili kwake in Manchester.

Aliandika: “Nimefika jijini Manchester kukamilisha details za ofa ya City.Kila kitu kipo sawa, muda mchache ujao nitawaambia zaidi.”

No comments:

Post a Comment