Search This Blog

Thursday, March 6, 2014

WIKI MOJA KABLA YA MECHI YAO - MASHABIKI WA LIVERPOOL WAMUITA MOYES "GENIUS WA SOKA"


Mechi yao inaweza kuwa wiki kadhaa mbele kutoka sasa, lakini mashabiki wa Liverpool tayari wameshaanza maandalizi ya mchezo dhidi ya Manchester United utakaopigwa Old Trafford March 16th.

Kwa mara ya kwanza katika kipindi cha muda mrefu, Liverpool wapo juu ya Manchester United katika msimamo wa ligi mpaka kufikia mwezi huu. Wakishika nafasi ya pili wakati kikosi cha David Moyes kikiwa nafasi ya 7.

Huku wakiwa na matumaini ya kubeba ubingwa mbele ya Chelsea, City - mashabiki wa Liverpool wapo katika hali ya kuwakejeli wenzano wa United, na sasa tayari wameshatengeneza bango kubwa la kumkejeli kocha wa mahasimu wao David Moyes.

Hili ndio bango linalosomeka 'David Moyes ni Genius wa Soka'



No comments:

Post a Comment