Search This Blog

Thursday, March 6, 2014

MOURINHO: WACHEZAJI WA MADRID WANAJALI ZAIDI MUONEKANO WAO KULIKO KUSHINDA VIKOMBE


Kocha wa Chelsea Jose Mourinho amesema kwamba wachezaji wa klab yake ya zamani ya Real Madrid wanajali zaidi kuhusu muonekano wao hadharani kuliko hata kushinda makombe.

Kocha huyo mreno ambaye aliondoka Madrid na kurudi Chelsea baada ya kukaa Santiago Bernabeu kwa misimu mitatu amesema hakuwa anapendezewa na tabia hiyo wakati yupo kwenye klabu hiyo.

"Mara nyingi pale Real Madrid, wachezaji utawakuta kwenye vioo kabla ya mchezo ya mchezo wakati refa anawasubiri kuelekea uwanjani," Mourinho aliliambia gazeti Esquire.

"Lakini hivi ndivyo ilivyo jamii ya vijana wa siku hizi. Vijana wanajali sana kuhusu muonekano wao, wapo katika miaka ya 20 na mie 51 na ikia unataka kufanya kazi na watoto inabidi uielewe dunia yao.

No comments:

Post a Comment