Search This Blog

Tuesday, March 4, 2014

TAKWIMU YA SIKU: REKODI YA UFUNGAJI MABAO YA SUAREZ NA STURRIDGE NDIO BORA KATIKA HISTORIA YA EPL TANGU 1965

Rekodi za ufungaji wa mabao wa washambuliaji wa Liverpool Luis Suarez na Daniel Sturridge msimu huu ni bora kuliko zote katika ligi kuu ya EPL tangu msimu wa  1965.
Suarez na Sturridge sio tu kwamba wanaongoza kwa ufungaji wa mabao na kushika nafasi mbili za juu katika msimamo wa ufungaji katika EPL, lakini hawa ndio washambuliaji pea ambao wamefunga mabao angalau mabao 18 kila mmoja katika hatua hii ya msimu tangu walipofanya hivyo washambuliaji wawili wa Blackburn  Andy McEvoy na John Byrom mnamo mwaka 1965.
Mpaka wakati timu zikiwa zimecheza mechi 28, McEvoy alikuwa kashafunga mabao 25 wakati John Byrom alikuwa kashafunga mabao 18. 
Suarez mpaka sasa kashafunga mabao 24 na Sturridge 18.

No comments:

Post a Comment