Search This Blog

Friday, March 7, 2014

RASMI : EMAD MOTEAB KUIKOSA YANGA NA KIUNGO HOSSAM ASHOUR AGOMA KUONGEZA MKATABA.


KIKOSI cha Al Ahly kimeanza kupata pigo kabla ya kuwavaa Yanga baada ya kiungo wake Hossam Ashour kugoma kuongeza mkataba huku mshambuliaji Emad Moteab akiondolewa katika orodha ya nyota 23 walioingia kambini jana kujiandaa na mchezo huo.

Taarifa ambazo zimetolewa jana na klabu hiyo zimeleeza kwamba Ashour ambaye licha ya kugoma kuongeza mkataba atakuwemo katika mechi dhidiya Yanga amegoma kuongeza mkataba mpya wa kuendelea kusalia katika timu hiyo ambapo wachambuzi wanadai hilo limesababishwa na hali mbaya ya kifedha inayoiandama timu hiyo kwasasa.

Kiungo huyo ambaye taarifa zake zimeleta mshtuko mkubwa katika kambi ya Ahly, amewaambia hata saini mkataba kwasasa akiwataka kusubiri mpaka mwisho wa msimu huku taariofa zikienea kwamba ameshasaini mkataba wa awali na klabu ya Gulfs  ambayo haijajulikana mara moja ni timu kutoka Saudi Arabia au Falme za Kiarabu.

Wakati hali ikiwa hivyo kocha mkuu wa Ahly Mohamed Yousef ametangaza nyota 23 waliotangulia Alexandria kuweka kambi ya masaa 48 kabla ya mchezo bila ya mshambuliaji wao Moteab ambaye bado ni majeruhi.

Nyota huyo ambaye pia aliukosa mchezo wa kwanza uliopigwa wiki moja iliyopita jijini Dar ambao Ahly ilichapwa kwa bao 1-0 kikubwa akiwa na maumivu ya mgongo ambayo bado hajaweza kuwa sawa.

Taarifa hizo za kukosekana kwa Moteab ni habari njema kwa kocha wa Yanga Hans Van Pluijm ambaye mara kwa mara amekuwa akimhofia zaidi ambapo mshambuliaji huyo ni hatari kwa kuwahadaa mabeki wa timu pinzani.

Wakati huohuo uongozi wa Ahly umelazimika kuwapoza nyota wao kuwa kupawa posho kabla ya mchezo huo ambapo taarifa kupitia Abdel -Hafiz ambaye ni Mkurugenzi wa Ufundi amesema wamelazimika kuwalipa wachezaji wao kiasi cha Paundi 10000(Sh milioni 2.2) ikiwa ni sehemu ya mishahara yao ya mwezi kutokana na ukata mzito unaowakamili.

No comments:

Post a Comment