Search This Blog

Friday, March 7, 2014

ARSENAL WATAKA FIDIA YA PAUNDI 600,000 KWA FA BAADA YA WILSHARE KUUMIA AKIICHEZEA ENGLAND


Katika mkutano wa waandishi wa habari Ijumaa ya leo, meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amekiri kwamba Jack Wilshare atakuwa nje ya dimba kwa wiki 8 baada ya kuvunjika mguu.

Kiungo huyo kinda wa Arsenal hivi sasa ana mashaka kama atakuwemo katika kikosi cha ENGLAND kitakachoenda World Cup, huku kukiwa na uwezekano mdogo wa kucheza katika msimu huu wa ligi tena ambao upo mwishoni.

Kwa mujibu wa gazeti la The Sun ni kwamba Arsenal leo wametuma barua rasmi kwenda FA wakidai fidia ya £600,000 baada ya Wilshere kupata majeruhi hayo akiwa anaitumikia England katika mchezo wa ushindi wa 1-0 dhidi ya Denmark.

Arsenal wanasemekana wameudhika kwamba mchezaji huyo ambaye amekuwa akiandamwa na majeruhi aliachwa aendelee kucheza hata baada ya kuumia.

No comments:

Post a Comment