Search This Blog

Wednesday, March 5, 2014

ILIKUWA NI MAAJABU ZAMALEK KUKATALIWA BAO KWENYE UWANJA WAKE WA NYUMBANI-ATHUMANI MACHUPPA.


 " Mechi ambayo siwezi kuisahau katika maisha yangu ni ile ya Simba dhidi ya Zamalek, kule Misri. Ukitoa maandalizi yetu kuelekea katika mchezo ule. Wachezaji tulifanya kazi kubwa uwanjani. Mechi ilikuwa ngumu tangu mwanzo na jamaa ( zamalek) wakapata bao ila maajabu mwamuzi alikataa. Ilikuwa katika dakika kama ya 23 hivi, Matola alijifunga wakati akijaribu kuzuia mpira wa krosi. Ilikuwa ni maajabu waarabu kukataliwa bao katika uwanja wao. Tukajua ilikuwa ni nafasi yetu. Hatukupata muda wa kupumzika uwanjani. Muda wote tulikuwa tukikimbizwa. Walipopata bao tukajiambia wasipate lingine. Tukafika katika mikwaju ya penati tukiwa hoi, ila tukashinda mechi. Zamalek Vs Simba, 2003 ni mechi ngumu kuwahi kucheza katika maisha yangu ya soka "

No comments:

Post a Comment