Search This Blog

Saturday, March 1, 2014

MANUEL PELLEGRINI KUKAA JUKWAANI MECHI YA MARUDIANO DHIDI YA BARCELONA


Kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini amefungiwa mechi mbili na UEFA asisogelee eneo la kiufundi la uwanja kwa kumlaumu mwaamuzi baada ya klabu yake kufungwa na Barcelona katika michuano ya klabu bingwa ya Ulaya.

Pellegrini alisema baada ya timu yake kushindwa 2-0 nyumbani kwamba mwaamuzi kutoka Sweden Jonas Eriksson "hakuwa mwaadilifu kwa timu zote mbili".

Alituhumiwa kwa ukosefu wa nidhamu na amepewa adhabu ya kukaa jukwaani pamoja na mashabiki katika mchezo wa pili wa michuano hiyo na Barcelona mnamo Machi 12, pamoja na mechi nyingine za ziada.

No comments:

Post a Comment