Search This Blog

Friday, February 28, 2014

HUYU NDIO ALEN HALILOVIC - MRITHI WA MESSI NDANI YA FC BARCELONA - AZITOSA SPURS NA MAN UNITED AENDA CAM NOU


Baada ya miezi kadhaa ya tetesi juu ya atma yake itakuwa wai, kinda la klabu ya Dinamo Zagreb mwenye miaka 17 Alen Halilovic hatimaye ameamua timu ya kujiunga na kucheza soka na uamuzi aliochukua ni habari mbaya kwa vilabu vya Arsenal, Man United na Tottenham.

Badala ya kuchagua kujiunga na vilabu hivyo kutoka EPL, usiku wa jana kiungo huyo kinda wa timu ya taifa ya Croatia aliandika kupitia akaunti ya instagram na kuthibitisha kwamba anajiunga na klabu bingwa ya Spain FC Barcelona.

Halilovic, ambaye ni kiungo mshambuliaji amekuwa akifuatiliwa na vilabu vingi vya bara la ulaya kutokana na kipaji kikubwa alichokionyesha kiasi cha kuitwa 'New Messi'

Kupitia akaunti yake ya Instagram aliandika: Thanks Dinamo Zagreb for everything!!My first club and biggest love!!Now is time to move on to Barcelona ❤️

Halilovic anategemewa kujiunga na Barcelona mwishoni mwa msimu huu na ataanza kuitumikia Barcelona B.

ANGALIA UWEZO WA KINDA HUYU KISHA TOA MAONI YAKO ANASTAHILI KUITWA MESSI MPYA

1 comment:

  1. The way he plays just like MESSI..... welcome camp nou

    ReplyDelete