Search This Blog

Monday, February 10, 2014

MALINZI AMEWACHUKUA WATOTO WA SIMBA NA KUWAPELEKA NYUMBANI KWAKE?

Na Baraka Mbolembole
Mabepari wapo kila mahali, pia wana misingi mikubwa ya kifedha, na mahusiano makubwa na vyombo vya umma. Kwa mfano wana uhuru wa kutumia vyombo vya habari. Ila kama kiongozi anakuwa akiwavutia watu, basi ni kwa sababu ni kwa sababu yeye mwenyewe amavitiwa na hiyo kazi iliyo mbele yake. Watu ndiyo nguvu pekee inayoweza kusaidia mabadiliko. Hivyo kiongozi anatakiwa kuwaunganisha watu na kuwafahamisha kwamba umoja wao utasaidia kupata wanachotaka. Ila watu nao wanatakiwa kuamka.

Katika soka la Tanzania,  tunaweza kusema kuwa tumempata mtu ambaye tulikuwa tukimuhitaji, kwani  rais wa sasa wa Shirikisho la Soka Nchini, TFF, Ndugu, Jamal Malinzi  anaijua Jiografia ya Tanzania, na analifahamu vizuri soka la nchi hii.  Hivyo atakuwa anafahamu mahitaji  na mawazo yanayotakiwa ili kukuza mpira wa Tanzania. Malinzi licha ya kutajwa kama kiongozi hodari baada ya kupita kwa zaidi ya siku 100 za utawala wake, ameonesha kuwa muhubiri hodari shupavu, na bila shaka atakuwa mwanafunzi hodari pia. Na hili litawezekana endapo ataamua kutumia muda wake kutazama na kujifunza zaidi kuhusu nini hasa kinachotakiwa kuanza ili kupata msingi imara wa mpira wetu.

Soka mara zote linakuwa na mahitaji ya muda mfupi na muda mrefu. Malinzi ameingia na mipango yake, huku soka la vijana likiwa kipaumbele kikubwa kwake, na hapo Academy za soka anaamini ndiyo suluhisho la kwanza. SAwa ni jambo zuri kwa kuwa ameingia huku akiwa na kiu ya kufanikisha mipango aliyojiwekea. Sera yake kuhusu soka la vijana ni nzuri, na ziara yake aliyoifanya siku za nyuma katika Academy ya Allience Sports ya jijini Mwanza, ilirutubishwa na maneno mazuri kuwa hapo ndiyo kutakuwa kitovu cha mpira wa Tanzania. Hadi sasa Malinzi ameonesha kuwa mtu anayependa sana kazi yake, ila mikakati yake ni lazima iendane na uhimarishaji wa soka la mitaani.

Jiografia ya Tanzania, bado mchezo wa soka unahitaji unahitaji kuwekewa mkazo mkubwa sana katika ngazi za chini, kata, tarafa, wilaya na mikoani, kwa kuwa uchumi wetu hauwezi kuendana na mkakati wa Academy kwa nchi nzima. Vipaji ni vingi sana nchini. Labda huu ni wakati wa kuanzisha ligi za vijana ambazo muendelezo wake utakuwa hadi ngazi ya Kitaifa, kwa kuwa na michuano inayotambulika na si hii ya muda mfupi kama ilivyo Copa Coca Cola. Mfano michuano hiyo ya Copa, inaweza kufanyika kwa kipindi cha mwaka mzima kwa mtindo wa ligi. Ni ghali sana, ila udhamini ambao makampuni yanapewa katika soka la Tanzania unatakiwa kuendana na hali halisi. 

Mitaani, ndipo soka linapotoka. Ndiyo maana WAingereza wanataka kuhamia na kuweka nguvu zao zaidi katika soka la mitaani kuliko lile la mfumo wa Academy. Muundo mzuri wa mfumo wa soka uhusishe pia namna ya kuendeleza vipaji ambavyo kimsingi haviwezi kupata nafasi katika Academy kuwa kuwa mambo ya uchaguzi huendana na ukiritimba mkubwa kila mahali. Uzuri wa Academy ni kwamba vijana watakuzwa na kuendelezwa katika mwendo mzuri wa kinidhamu, kutambua majukumu na kuwajibika, ila siku zote ni lazima tutambue kuwa, kila mtoto huzaliwa na tabia njema, tabia mbaya huja baadae. UNaweza kuzalisha wachezaji 100 bora katika nchini na kujona umefanikiwa sana, ila tabia zao kadri wanavyokuwa wakikua zinakuwa zikibadilika. Soka la Academy ni muhimu, ila soka la mtaani ni tumaini la muda wote kwa mpira wa Tanzania.

Majuzi nilikuwa nikiwasiliana na James Julius,  Mtanzania ambaye yupo nchini Afrika Kusini, akifanya kazi katika Academy ya ' Stars of Africa'. Naye ameanza na mikakati ya kufanya uwekezaji katika soka. Ameomba ekali zaidi ya 20 katika mji wa Mwanza ili kuanza ujenzi wa ' Mandozi Sports Academy', maombi yake hayo anataraji kupata majibu mwezi huu. Huyu ni kijana mdogo tu na tayari ametumia zaidi ya millioni 20 kwa kuanzisha timu nne za vijana, U20, U17, U14, na U12. Mimi alinipatia CD za hiki ninachokisema hapa na nimeona mikakati yake. Hivyo kwa Malinzi, bila shaka tayari ametoa mwamko na matumaini kuwa watu wamemuelewa na tayari wanatumia nguvu zao kusaidia soka la Tanzania

Hapa ni makampuni yanayotakiwa kusaidia katika ili na si kusubiri kujitokeza hapo baadae wakati wakiona kuna matunda ya wao kutangaza biashara zao. Makampuni mengi yamekuwa yakijinifaisha kupitia ufadhili wao katika soka la Tanzania, Hata udhamini wanaoupata timu zetu mbili kubwa kwa sasa hauendani na thamani ya klabu hizo. Simba na Yanga zinawaingia faida kubwa wadhamini wao kuliko kile wanachoingiza wao kutokana na ufadhili au udhamini walionao. Makakati, wa Mandozi, Sports Acacemy, Allience Sports Academy unatakiwa kusapotiwa kwa nguvu na makampuni yaliyopo nchini. Yatafikaje, ni kwa wahusika wenyewe kujitokeza na kuonesha kuwa wapo tayari kufanya kitu kikubwa hivyo wanatakiwa kuyafuata makampuni hayo na kuyaomna yaende kuwasaidia.

  WANAOSEMA TFF IMEJAA, U- SIMBA NA U-YANGA NAWASHANGAA

Hivi ni nani anayeweza kuishi nje ya fikra za Simba na Yanga? Labda kwa yule ambaye si mpenzi wa soka. Wakati mwingine sisi binadamu tunakuwa wanafiki kweli. Nani hajui kuwa Jamali Malinzi amewahi kuwa kiongozi wa juu wa klabu ya Yanga? Nani hajui kuwa Geofrey Nyange Kaburu amewahi kuwa kiongozi wa juu wa klabu ya Simba> Vipi kwa kina Abbas Tarimba, Seif Ahmed, David Mosha, Zacharia Hans Poppe, Clement Sanga, mimi ninafikiri muhimu ni kuwashauri kuwa mpira wa Tanzania unawategemea sana wao hivyo wanatakiwa kufanya kazi zao kutokana kanuni na taratibu zilizopo. Wasiweke mapenzi ya vilabu vyao katika mambo muhimu.

Mimi, wewe, sote tumekuwa na upenzi wa soka. Inategemea tu, wewe utakuwa unaangukia wapi katika mapenzi yako, inaweza kuwa Simba, au Yanga ama timu nyingine yoyote ile. Ndiyo, Malinzi amewavuta watu wengi wa Simba na Yanga katika kamati zake, ila si kwa lengo la kuharibu mpira bali kupanga na kusimamia vuzuri mikakati inayoweza kusogeza soka la Tanzania mbele zaidi. Ni makosa kumuhukumu kwa sasa ila hatutosota kumsema vibaya endapo tunashuhudia kamati zake zikifanya mambo kwa kuvutana kisa mapenzi ya u- Simba na u- Yanga. Kwa sasa tuwasisitize wafanye kazi zao vizuri bila kusukumwa na ushabiki na si kuwahuku kwa makosa yasiyokuwepo. Kama hatuwataki hao, kisa ni Simba na Yanga, mleteni basi Sir Alex Ferguson aje kuwa rais wa TFF, kwa kuwa watu wengi wa soka wanatoka katika mapenzi ya dhati ya Simba na Yanga.

Itakuwa ni makosa makubwa kwa Malinzi, endapo watu aliowaamini na kuwapatia nafasi watamuangusha kisa ushabiki wa klabu zao. Itakuwa ni sawa na muwindaji ambaye aliamua kuchukua mtoto wa Simba na kumpeleka nyumbani kwake. Huyu atakuwa amejipelekea maangamizi yeye mwenyewe na familia yake. Soka la Tanzania halihitaji wafanyakazi wa mapenzi, ila ukweli ulio wazi linawahitaji watu waliopita Simba au Yanga, iwe kiuongozi au kiuchezaji. Mkakati wa Malinzi na soka la Tanzania unahitaji fikra zetu sote. Kulaumu kupo tu kila mahali, ila nasi tutoe ushauri mzuri kwao ili kwenda sambamba na matarajio yanayokusudiwa. Nimewasilisha tu. Karibuni pia Mandozi Sports Academy...

7 comments:

  1. Kuwashangaa wanaokosoa soka la nchi hii hasa uongozi wake kujaa usimba na uyanga; sio tu unawashangaa, bali, ni lazima uwashangae kwani akili na mawazo yako yameumbiwa katika mkondo wa fikra mfungo, ambao moja ya tabia zake ni kushangaa hata lilo na uhakiaka ama ukweli. Nadhani fikra zinalenga kutetea kile ambacho kwa uwezo wake inaonekana ni sahihi hata kama si sahihi. Sio kweli kwamba kila mtanzania mwenye kupenda soka kaumbiwa katika fikra za usimba na uyanga. Kwa kauli hii ni kitu ambacho kitaalamu kinaitwa "fallacy of generalization". Wapo wadau wengi wa soka katika nchi hii ambao kwao ukiwagusia suala la simba au yanga, hakika wanaweza kukutandika vibao, kwani vilabu hivi viwili ndivyo vinavyoharibu soka la nchi hii. Kwa mtu mwenye kupenda maendeleo ya soka yu lradhi kuona vilabu hivi pengine vikipotea katika ulimwengu wa soka nchi hii. Soka la nchi hii limegubikwa na tabia mbovu za usimba na uyanga ambao ndio kaburi la kandanda letu. Hakika unapomchagua kiongozi au mchezaji aliyewahi kuwa sehemu ya jamii ya vilabu hivi, hakika unazidi kulichimbia kaburi soka letu na hata siku moja hawatakuja kufanya maamuzi pasipo kuathiriwa na lahana ya timu hizi. Vipo vilabu vidogo vidogo na hata vingine viko ligi kuu, ambavyo viongozi wake wanauwezo mkubwa wa kuliongoza taifa hili pasipo kuwa na dhana ya usimba au uyanga, lakini jambo la kushangaza, kiongozi huyu ambaye anachagizwa na watanzania wengi hakujaribu kuwaona watu hawa zaidi alichokifanya ni kuleta wale ambao amezoeana nao na pengine kufanya nao kazi. Kinachotegemeawa ni nini kama si kuliangusha soka la nchi hii na siku zote tutazidi kupiga kelele lakini mchawi tunamjua wenyewe lakini tuna mfumbia macho. Tazama marefa wengi wa nchi hii wamekuwa wakiamua mechi za ligi kwa ushambiki wa simba na yanga. na hilo ni wazi kabisa kwani wameonekana kupindisha kanuni au kufanaya makosa mengine yanashangaza, hasa kwenye mechi za timu hizi mbili. Lakini marefa haohao, wanafanya vizuri wanapochezesha mechi ambazo simba na yanga hawahusiki.TFF hao wakawakoromea watu ambao wanawalaumu waaamuzi lakini bado hawawaonyi waamuzi hao hao. Kama si usimba na uyamga ni nini?

    ReplyDelete
  2. Utakuwa ni unafiki kusema tuwaamini malinzi na hao washikaji zake ambao walishika nyazifa mbalimbali katika simba na yanga.hao wote wapo hapo kwa ajili ya maslahi yao binafsi na si kwa ajili ya maendeleo ya soka la bongo,najua kwanini wanaojiita wadau wa soka la bongo hawataki kuona simba na yanga zinapata changamoto katika ligi kuu ya bara,kuanzia viongozi wa TFF hadi baadhi ya WAANDISHI WA HABARI ZA MICHEZO hapa bongo ambao wamekosa nia ya dhati katika kuripoti hali halisi na upuuzi tunaoletewa miaka yote na hizi klabu mbili ambazo binafsi naziona ndo kiini cha kudidimia soka letu,Ebu tujiulize huyo malinzi na hao wasanii wenzake aliowajumuisha kwenye kamati mbalimbali za TFF kipindi ambacho wapo simba na yanga walileta mabadiliko gani katika kuendeleza hizo klabu za kishamba? wakati umefika sasa tuache ujinga wa kuwaamini watu kama hao kizembezembe,ni jambo la kushangaza watu walioongoza simba na yanga miaka mingi iliyopita ambapo bado simba na yanga hadi leo hazina maendeleo yoyote ya kujivunia zaidi ya mataji ya ligi kuu bara ambayo tukiacha unafiki wamekuwa wakionga wachezaji wa timu pinzani pamoja na marefa,wakifika kwenye michuano ya klabu ya kimataifa ni aibu tupu,HIVI TFF HAIWEZI KUONGOZWA NA WATU WENGINE MAKINI HADI TUWACHAGUE HAO WALIOTOKA KUVURUNDA KWENYE KLABU ZA WASHAMBA ZA SIMBA NA YANGA? Binafsi naona hakuna umakini wowote kwenye hili na hao wajumbe wa TFF ni tamaa za kipuuzi tu zinazowafanya watuchagulie viongozi mizigo.siungi mkono hata kidogo kuturudishia akina ABBAS TARIMBA kwenye zama hizi ambazo wapo watu makini wanaoweza kutufikisha pale tunapohitaji,TFF IMEJAA USIMBA NA UYANGA NA SISI WAPENDA MAENDELEO YA SOKA LA BONGO TUNAKUSHANGAA WEWE AMBAYE UTAKI KUKUBALI UKWELI KWAMBA SIMBA NA YANGA NI GONJWA SUGU KWENYE SOKA LA BONGO,mabadiliko na maendeleo yatapatikana mkiacha kulazimisha kuzisifia kijingajinga.

    ReplyDelete
  3. Nmekuelewa baraka. To tell the truth, hiwezi kutenganisha soka la nchi hii na simba na yanga. Anyone antajie just kiongoz mmoja ambaye hayupo upande wowote... Na ukickia kiongoz anasema yupo neutral, utagundua ni mnafki 2. Waulize watu wake wa karibu watakwambia... Itz hard truth 2 swallow bt u hav 2.. Kinachotakiwa ni kwa hao viongoz kuelewa kuweka boundaries kati ya kazi na mapenzi binafsi, na inawezekana coz sidhan kama sepp blatter hapend mafanikio ya sweden national team. Bt ni lazma afanye kaz yake... Watu wa mpira ndo hao hao, unamteua nan mwngne? May b tuchukue watu wa basketball waongoze mpira wetu.

    ReplyDelete
  4. Yani katika watu wanaojisemea ovyo ni pamoja na huyu jamaa mchangiaji wa kwanza anayesema eti Simba na Yanga ndo wanaharibu soka la tanzania. Haya ni maneno ya kijinga ambayo yamezoeleka kutamkwa na watu wa hovyohovyo bila kuzingatia ukweli halisi. Nawachukia sana vilaza wa namna hii. Wengi wao wanaugonjwa unaojulikana kitaalamu kama "cognitive disonance"

    ReplyDelete
  5. Mwalimu Nyerere aliwashangaa viongozi aliowaachia nchi kwa kuchukua mambo mabaya aliyoyafanya katika uatawala wake na kuyaacha yale mazuri.Mfano huu unamhusu Malinzi ambaye badala ya kuchukua mazuri yaliyofanywa na Tenga ameamua kukumbatia makomandoo wa Simba na Yanga na kuwajaza kwenye kamati zake na sasa wameanza kumpa ushauri wa kipuuzi na yeye kuukubali kama ule wa kuacha kutumia tiketi za elektroniki.Sio kweli kwamba nchi hii watu wanaojua mpira ni wale waliowahi kuongoza Simba na Yanga tu.Wako watu wengi wameongoza vilabu na vyama vya mpira nje ya simba na yanga kama Mbeya City,Kagera Sugar,Majimaji,Coastal Union,JKT Ruvu,Mtibwa n.k na unahitaji kuwa makini lil kuwapata vinginevyo utakurupu
    kia watu wale wale wa kila siku kama Tarimba,Dalali,Hanspope,Madega,Sauko n.k ambao hakuna lolote walilofanya la maendeleo ya soka kwenye klabu zao.Hawa ndio wameharibu huko na sasa wanaaminiwa kwamba eti watalikomboa soka la nchi hii kupitia kamati za TFF.Malinzi mwenyewe sio mtu wa soka ni mbabaishaji(opportunist) aliyetokea kwenye upromota wa ngumi za kulipwa aka"chance" kuingia kwenye soka mwanzoni mwa miaka ya 2000 kwa nguvu ya fedha zake na kupitia makomandoo wa Yanga lakini leo hii anaonekana ndiyo suluhisho la soka la Tanzania akiwazidi watu aliowakuta kwenye soka kama kina Tenga,Nyamlani,Angetile n.k.HIVI UNATARAJIA MAENDELEO GANI YA SOKA KUTOKA KWA MADEGA AMBAYE MWAKA 2008 ALIDIRIKI KUZUIA TIMU ISENDE UWANJANI KUCHEZA MECHI YA KOMBE LA KAGAME KWA SABABU ZA KIPUUZI,LEO HII NI KIONGOZI WA KAMATI MUHIMU YA TFF.Hivi huyo Dalali na Hanspope si walizuiwa kugombea uongozi Simba kwa kukosa siafa za kikatiba lakini leo hii ni viongozi wa soka wa kitaifa kupitia kamati za TFF.Haya hao kina Tarimba,Sauko n.k si ndio hao hao miaka nenda miaka rudi wamevuruga soka la Tanzania kwenye ngazi ya klabu? Malinzi aliahidi kuileta mabadiliko kwenye uendeshaji wa soka lakini KAANZA NA MGUU MBAYA kwa kujaza makomandoo walewale wa simba na yanga kwenye kamati zake huku wakimpa ushauri wa hovyo na yeye anakubali

    ReplyDelete
  6. Bw. J. Malinzi anaonekana kua kiongozi bora, na anaonekana kua na nia dhati kabisa ya kuukwamua ama kuuendeleza mchezo wa mpira wa miguu Tanzania. Ombi langu ni kua aache kusikiliza ama kufuatilia maneno maneno ya watu, afanye kazi na sio kusikiliza nani kasema lipi na yupi kasema lipi juu yake.mfano mbona Mheshimiwa raisi wa nchi amekua akishutumiwa kila kona anawatoto ama ata akiteua mwanamke ktk nyadhifa za uongozi watu wamekua wakidai kua ni awala yake ama aliwai kua kimada wake, lkn je ashawahi kujibu shutuma hizo...ukweli sijawahi sikia akijibu na hii imekua ikimfanya awe huru na kusonga mbele.

    Nakusihi Malinzi waache wapige mayoe wakichoka waataacha, na hakika hata ukitaka kuwaweka sawa hutoweza maana wapo wengi wasio penda mafanikio ya mtu aliye onesha nia. alishindwa yesu utakua wewe bwana. Piga kazi tubadilishe soccer ya nchi yetu.

    ReplyDelete
  7. Malinzi na Kikwete wapi na wapi?,Malinzi hajui mpira na anaongozwa badala ya kuongoza.Kila ushauri wa kijinga anaopewa anaufanyia kazi matokeo yake kamaliza siku 100 hana cha kujisifu zaidi ya kuanza kuwalaumu kina Tenga kwa kumuachia madeni

    ReplyDelete