Search This Blog

Monday, February 10, 2014

FAHAMU SABABU YA ULINGO WA PEMBE NNE KUITWA ‘BOXING RING’

Na Arone Mpanduka,Radio Tumaini
MCHEZO wa ngumi ni sanaa ya ulinzi binafsi baina ya mtu ambaye anatumia mikono yake miwili katika mapigano ambapo kwa lugha ya kigeni wanasema "the manly art of self-defense"
Mchezo huu ulianza katika karne ya 17 na kuanza kufahamika katika karne ya 18 huku chimbuko lake likiwa nchini Ugiriki.
Ngumi ulikuwa ni mmoja kati yak michezo ya mwanzo kuingizwa katika mashindano ya Olimpiki katika miaka ya 688 BC.
Wakati huo mabondia walikuwa wakipigana kiholela bila sheria na kanuni za kueleweka sanjari na vifaa duni vya kupigania.
Wagiriki waliweza kubuni gloves za aina yake ambapo walianza kuvaa ngozi za wanyama kwenye mikono yao zilizokuwa zikifahamika kama cesti.
Lakini kuna mabondia wengine walikwenda mbali zaidi na kuchomeka vitu vyenye asili yak chuma katika ngozi hizo na kuleta madhara makubwa kwa wapinzani wao wakati wa mchezo kwani vyuma hivyo vilikuwa vinajeruhi vibaya na hata kusababisha kifo kwa mpinzani.
Baada ya kugundulika kuwa ni mchezo wa hatari ililazimika kuufungia kwa muda kabla yak kuibukia katika nchi zingine ikiwemo Uingereza pamoja na nchi nyinginezo.
Nchini Uingereza bondia James Figg aliweza kutamba na mkanda wa uzito wa juu kuanzia mwaka 1719 hadi 1730.
Mchezo huo ulizidi kukua na kuenea nchi mbalimbali duniani huku sheria na kanuni zikitengenezwa na kuboreshwa na baadae kuufanya kuwa mchezo wa kisasa.
Hivi sasa ngumi imekuwa na majina mengi kama vile masumbwi, ndonga, ndondi, mkono, vitasa na wengine hudiriki kuita mawe.
AINA ZA MCHEZO HUO
Mchezo wa masumbwi umegawanyika katika aina kuu mbili ambapo ni pamoja na ngumi za ridhaa na zile za kulipwa(Amateur and Professional)
Licha ya kuwepo kwa aina hizo kwa ujumla mchezo huu una wastani wa kuchezwa katika raundi 12 ambapo kila raundi ina muda wa dakika tatu na kila baada ya raundi moja mabondia hupumzika kwa dakika moja.
Pia ipo michanganuo mbalimbali ua uzito ambayo bondia hushindana kulingana na uzito alio nao kama vile Flyweight (50.8 kg); Bantamweight (53.5 kg); Featherweight (57.2 kg); Lightweight (61.2 kg); Welterweight (66.7 kg); Middleweight (72.6 kg); Light Heavyweight (79.4 kg) pamoja na Heavyweight.
ULINGO WA MASUMBWI
Kama ilivyo katika michezo mingine ambayo lazima iwe na uwanja wa kuchezea, katika masumbwi nako uwanja wake upo ambao ni ulingo.
Ulingo huwa na pembe nne zenye kuzungushiwa kamba ngumu pembeni yake na huusisha watu watatu ndani yake yaani mabondia wawili na mwamuzi.
Nje ya ulingo mwamuzi husaidiwa na majaji watatu ambao nao huutazama mchezo na kila mmoja kutoa alama zake.
KWANINI UITWE BOXING RING?
Watu wengi wamekuwa wakitamka neno la Boxing Ring wakimaanisha ulingo wa masumbwi wakati kimuonekano ulingo huo una pembe nne.
Kama inavyofahamika, maana halisi ya ring ni pete ambayo mara zote huwa na umbo la duara.
Ukweli ni kwamba katika karne ya 18 na 19 mabondia wengi walikuwa wakicheza pambano hilo huku wakiwa na vifaa duni ikiwemo ukosefu wa gloves, sare na hata ulingo wa kuigania.
Kilichokuwa kinafanyika ni kwamba mwamuzi wa mchezo anachukua kijiti na kisha anachora duara kubwa ardhini na kisha mabondia huingia ndani yake na kupigana huku watazamaji wakizunguka duara hilo.
Hapo ndipo neno Boxing Ring ilipoibuka kwasababu mabondia walikuwa akipigana kwenye uwanja wa duara.
Mazoea hayo yaliendelea kuchukua nafasi hata ilipofika kipindi ambacho ukagunduliwa ulingo wa pembe nne ambapo bado mashabiki wakaendelea kuuita Boxing Ring.
Ulingo wa kwanza wa pembe nne ulibuniwa na jamii ya watu wa Pugilist mnamo mwaka 1838 ambao ulikuwa na eneo la ukubwa wa mita 7.3 za mraba.
0786160643

No comments:

Post a Comment