Search This Blog

Thursday, February 20, 2014

FABREGAS AOMBA RADHI KWA NIABA YA BARCELONA KUIFUNGA MANCHESTER CITY.

 Kiungo wa FC Barcelona Cesc Fabregas ilimbidi awaombe radhi mashabiki waliohudhuria tuzo za Uingereza kwa niaba ya klabu yake ya Fc Barcelona.
Fabregas ilimbidi aombe radhi baada ya mashabiki hao kuanza kumzomea pale alipopanda jukwaani kutoa tuzo ya kikundi bora cha kimataifa,akiwa jukwaani na mwanamuziki Nicole Scherzinger ndipo kelele za kumzomea zilipoanza kusikika ukumbini hapo na yeye bila kuchelea aliwajibu '' samahani sana kwa yaliyotokea jana,nimekuja hapa kwa amani kabisa'' alizungumza Fabregas kabla ya kuwatunuku tuzu hiyo wasanii wa kikundi cha Daft Pun.
 Tuzo hizo zilifanyika jijini London kwenye ukumbi wa O2 Arena.
   Fabregas akiwa na mwanamuziki Nicole Scherzinger....
 Fabregas akitoka Hotelini jijini Manchester na wachezaji wenzake mara baada ya mchezo dhidi ya  Man City kurejea nchini Hispania,lakini yeye alimbidi aende jijini London kuhudhuria tuzo hizo.
Fabregas kushoto akishangilia na wachezaji wenzake bao la kwanza la Mesii kwenye mchezo dhidi ya Man City.

No comments:

Post a Comment