Search This Blog

Thursday, January 9, 2014

UCHAGUZI WA TASWA FEBRUARI 16...



UCHAGUZI Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), unatarajiwa kufanyika  Februari 16 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Uamuzi huo umefikiwa na kikao cha Kamati ya Utendaji ya TASWA  kilichofanyika Dar es Salaam jana kujadili masuala mbalimbali ya chama na waandishi wa habari za michezo kwa ujumla.

Kikao kilikubaliana kuwa uchaguzi ufanyike kwa katiba ya zamani, kwani mchakato wa katiba mpya unaweza kuchukua muda mrefu, hivyo kusababisha viongozi waliopo madarakani kuendelea kukalia viti kinyume cha katiba, jambo ambalo si sahihi.

Kutokana na hali hiyo viongozi wapya watakaochaguliwa moja ya kazi yao kubwa itakuwa kuifanyia marekebisho makubwa katiba ya chama ili iende na wakati.

BOFYA HAPA CHINI KUMSIKILIZA AMIR MHANDO KATIBU MKUU WA TASWA.

No comments:

Post a Comment