Search This Blog

Monday, January 13, 2014

MALINZI KUTEMBELEA KITUO CHA ALLIANCE

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi atafanya ziara ya siku moja kutembelea kituo cha mpira wa miguu wa vijana cha Alliance cha jijini Mwanza.

Lengo la ziara hiyo ni kuangalia jinsi Alliance inayoendesha shughuli zake ili Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) liweze kushirikiana na kituo hicho kwa karibu.

Rais Malinzi katika ziara hiyo atakayoifanya keshokutwa (Januari 15 mwaka huu) atafuatana na Mwenyekiti wa Kamati ya Mpira wa Miguu kwa Vijana, Ayoub Nyenzi na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Ramadhan Nassib.

Alliance inatarajia kufanya mashindano yatakayoshirikisha vituo vyote vya kuendeleza mpira wa miguu kwa vijana (academy) wiki ya tatu ya Februari mwaka huu jijini Mwanza.

Mashindano hayo yatashirikisha timu za umri wa miaka 13, 15 na 17 ambapo Alliance itagharamia malazi, chakula na usafiri wakati timu hizo zikiwa jijini Mwanza.

No comments:

Post a Comment