Gaucho mwenye umri wa miaka 33
amesaini mkataba wa miaka 2 na nusu kujiunga na Besiktas inayoutumia uwanja wa
BJK İnönü,taarifa hizi zimedhibitishwa na gazeti la ‘De Telegraaf‘ la nchini
Uholanzi – inasemekana Ronaldinho atakuwa akilipwa kiasi cha kati ya Euro milioni
10 na 15 kwa mwaka.
Inasemekana sababu kubwa ya Ronnie
kuhamia tena ulaya ni kujaribu kurejesha kiwango chake ili aweze kumshawishi
kocha wa timu ya Taifa ya Brazil Luiz Felipe Scolari ili aweze kujumuisha jina
lake kwenye kikosi cha Brazil kinachotaraji kushiriki fainali za kombe la dunia
baadae mwaka huu.
Hivi karibuni gazeti la EL PAIS la
nchini Uruguay lilimtangaza Gaucho kuwa mwanasoka bora wa bara la Amerika ya Kusini
kwa mwaka 2013 baada ya kuiongoza timu yake ya Atletico Mineiro kutwaa kombe la
Copa Libertadores kwa mwaka 2013 ikiwa ni pamoja na kufunnga jumla ya mabao 17
na kutoa pasi za mwisho 11 kwenye jumla ya michezo 36 aliyocheza.
No comments:
Post a Comment