Search This Blog

Wednesday, January 22, 2014

BREAKING NEWS! USAJILI WA OKWI YANGA WADUNDA..

Taarifa ambazo mtandao huu umezipata hivi punde jina la Emmanuel Okwi halijaidhinishwa kwenye usajili wa klabu ya Yanga.
Kwa maana hiyo Okwi hataruhusiwa kucheza raundi ya pili ya Ligi Kuu ya Vodacom mpaka sakata lake la usajili kutoka klabu ya Etoile du Sahel litakapotafutiwa ufumbuzi.

Endelea kufuatilia mtandao huu kwa taarifa zaidi.......

7 comments:

  1. Shaffih dauda wewe ni mjanja sana tumeshakujua wewe ni Simba damu umetuzuga kwa highlight za mechi ya kirafiki ya Yanga uturuku halafu unatupiga kiboko kwa taarifa za okwi usajili wake yanga

    ReplyDelete
  2. Highlites cio highlight

    ReplyDelete
  3. Tanzania Football Fitina

    ReplyDelete
  4. Kama kawaida mambo ya usajili kwa hizi timu zetu ni issue,cheki watu wanamsajili mchezaji bila kuhakikisha kama hana mkataba na club nyingine.Timu zinasikiliza mchezaji hata kama ni muongo,Okwi hakusema kama ana mkataba kwa viongozi wa Yanga?Au hakutumia akili yake?

    Abraham J Mcharo

    ReplyDelete
  5. yanga wamezoea kiherehere, lengo lao ilikuwa kuwakomoa simba... acheni kubabaisha acheni fitina fanyeni football ichukue nafasi yake

    ReplyDelete
  6. Hizi taarifa nadhani zitasaidia kuwaelimisha na kuwafungua macho watu wa mpira pesa kina ustadh na wengine wote ambao wamekua wakimchafua Aden kwa kisingizio cha uongo eti amemuuza okwi na kupokea pesa toka Etoile,huo ni uongo na nyie waandishi muache kukubali kutumika kuchafua watu,Rage hajala hela za mauzo ya okwi na wala hajaziweka kwenye akaunti ya mkewe,na hili la okwi kuzuiwa kucheza limewezekana kwa jitihada zake,tuwe fair,tumpe credit zake inapobidi na tumkosoe inapobidi

    ReplyDelete
  7. Okwi ni mchezaji halali wa Yanga,na hata ukiangalia kwenye website ya Etoile du Sahel hakuna jina la Okwi katika orodha ya wachezaji wa timu hiyo.Kinachofanyika ni fitina za watu wa Simba walioko TFF hasa Kaburu na Kidau pamoja na Hanspope ambaye yupo kwenye hiyo kamati iliyomzuia Okwi.I ngewezekanaje shirikisho la soka la Uganda litoe ITC huku linajua kwamba Okwi ameruhusiwa kwa muda tu kuchezea Villa?halafu ITC si inatolewa baada ya TRANSACTIONS za uhamisho huo kukubaliwa katika mfumo wa TMS(Transfer matching system) ambao lazima uidhinishwe na FIFA?kinachoendelea ni kutaka kumchelewesha Okwi kuanza kucheza Yanga kama ilivyofanyika kwa Ngassa mwanzoni mwa msimu huu.

    ReplyDelete