Search This Blog

Friday, December 20, 2013

FUFA YAMUIDHINISHA RASMI OKWI KUCHEZEA YANGA



WAKATI straika mpya wa Yanga, Emmanuel Okwi akitua nchini tayari kuitumikia timu yake mpya, Shirikisho la Soka la Uganda (Fufa) limesema mchezaji huyo ni halali kuichezea Yanga na ndiyo maana walikubali kutoa hati ya uhamisho wa kimataifa (ITC).

Ofisa Mtendaji mkuu wa Fufa, Edgar Watson ameuambia mtandao huu kwamba, anachojua kama bosi wa Fufa ni kwamba ni kweli Okwi amesaini kuichezea Yanga na shirikisho lake limetuma ITC kwenda Tanzania kwa Yanga ili aweze kuichezea timu hiyo.
“Kwanza nataka kuweka wazi kwamba, Okwi alikuwa na kesi dhidi ya timu ya Etoile du Sahel ya Tunisia juu ya masuala ya mkataba, Fifa (Shirikisho la Soka la Kimataifa) lilimruhusu kucheza kwenye klabu ambayo anaitaka kwa muda maalum.

 


Okwi alipewa kibali maalum, hivyo si kweli kuwa alikuja kucheza SC Villa ya hapa (Uganda) kama mchezaji wa mkopo, huyu alipewa kibali maalum sasa hapo kuna tofauti ya kibali maalum na mkopo,” alisema Watson.

Alisema Okwi aliruhusiwa kucheza na Fifa na ruhusa ambayo amepewa haikuwa ikimzuia kuhamishwa au kusajili kwenda klabu nyingine, hakuna mahali anapozuiliwa kusajiliwa bali kilichofanyika ni sawa na ruhusa ya kucheza.
Watson alisema kilichotokea ni kati ya Villa, mchezaji na huko alikosajiliwa ni baina yao na hakuna kinachomzuia asisajiliwe.

“Kwa mazingira yaliyopo, hakuna kipengele chochote ambacho kinamzuia mchezaji mwenye ruhusa maalum kuhamishwa hivyo tumetoa ITC na hakuna ambacho kingemzuia Okwi kwenda kule anakotaka,” alimalizia Watson.

BONYEZA HAPA CHINI KUSIKILIZA MAHOJIANO YA EDGAR WATSON.

3 comments:

  1. Haya Bana, mi huwa nawakumbusha kuwa Tusitumie nguvu kubwa kutafasiri sheria wakati SISI sio Wanasheria. Hanspope alijiapiza kuwa Okwi hachezi yanga, alishawahi jiapiza Kwa Ngasa na hivyo kuwahadaa wanachama. Tatizo lipo kwenye taarifa ya kwanza iliyotolewa kuwa OKwi amesaini Villa kwa miezi sita. Haikutafasiriwa vizuri na sote tukaamini bila kufanya utafiti, Kumbe "Provisional" si Sawa na "Loan" na hicho ndicho kimetumiwa na akina Bin Kleb na Villa kumleta Okwi Tz.

    Waandishi tuwe makini na kutoa habari vizuri na kuweka kwenye mizani ili tuwe na picha halizi,

    Mambo ndo mambo na sasa kinaendelea kunuka kwa Rage, TFF wamekaa kimya ila angekuwa kaka yangu Angetile yeye Fasta kama anaona ukweli basi angetoa jibu lakini akina wamb.... mhhh.

    Kuna muandishi aliwahi kusema kitu kuhusu hili la Okwi sijui ni Salehe Ally. Sinema inaendelea.

    ReplyDelete
  2. mm nimehamia lipuli simba nimehama

    ReplyDelete
  3. Hapo juu mchangiaji wa kwanza, umeandika vzuri bt umekosea sehemu moja kumsifia mvurugaji, mwenye uwezo mdogo Angetile Osiah. Jifikirie mara mbili

    ReplyDelete