Search This Blog

Thursday, November 7, 2013

MAKALA HII NI KWA WALE WANAOMPONDA GIROUD


Imeandaliwa na Joel Chuku.



Mnaosubiri Giroud Awe Kama Kuni Aguero, Van Persie Au Suarez labda
Henry Mpya Mnajiongopea sana na mtahishia kumtukana Kila siku Giroud
Sio Style Ya Hao Watu Wala Mpira ule Hauwezi.. Na hili kujua uwezo wake
Lazima uwe unajua mpira

 Arsenal Ina Change Formation Kutoka 4-3-3 ambayo inahitaji uwe na
speed uwanjani na Kuwa 4-2-3-1 Giroud anacheza Kama ‘Lone Striker’
akipunguziwa movement uwanjani kutokana na uwezo aliojaaliwa na anaimudu
iyo nafasi kwenye huo mfumo.

 Kwenye mechi tuliyocheza na Norwich City, lile goli la wilshere Alilofunga la
kupigia pass nyingi, Wakati Giroud anapiga pass ya mwisho kwenda kwa
wilshere alikua katikati ya mabeki wawili akaipenyeza kwa Wilshere
aliyefunga akiwa free huku mabeki wote wakikimbilia kwa Giroud.

 Siku ile na Liverpool wakati Sagna anapiga krosi alikimbia kwa
Speed kwenda usawa wa golikipa huku mabeki Martin Skrter na Sakho wakiamishia akili zao kwa Sagna,
kitendo kilichopelekea wabeki hao kuacha nafasi katikati kwa Santi Cazorla mchezaji mfupi kupata nafasi ya kupiga kichwa huku akiwa peke yake tena akawahi mpira uliogonga Mwamba kasha akafunga.

 Kwenye mchezo wa kwanza tuliocheza na Dortmund Giroud alifunga bao akiunganisha krosi ya beki Bacar Sagna baada ya kukimbia kwa kasi na kumuacha beki Neven Subotic pamoja na golikipa wake.
 Goli la jana la Ramsey Giroud alitoa Pasi ya Kichwa akiwa katikati
ya mabeki wawili akawamudu akaudondosha mpira kidogo kwa Ramsey na
bwana mdogo akafunga....

 Goli alilokosa Ramsey Jana Giroud anapata mpira pembeni Defenders
wana mfu ata anaupiga mpira kule walipotoka Ramsey anakosa goli yeye na
kipa..

 Giroud hawezi kumpunguza beki akiwa na mpira mguuni mwake ila movement
zake akiwa hana mpira na uwezo wa kukaa kwenye position akiwa hana
mpira ndio zinaleta umuhimu wake, hawa akina Ramsey wasingekua
wanafunga hivi kama mngetaka Giroud acheze kama akina tevez..

Giroud is more like holding striker than direct striker, Tunahitaji
Striker Mwingine World Class Ambae atakua ana uwezo wa kuwatazama mabeki
ili awe ana utofauti na Giroud ili aweze ku-offer kitu kingine kwenye
team tuwe na uwezo wa kutumia hata strikers wawili wenye uwezo tofauti
kama ikihitajika kufanya ivyo ila sio kweli kwamba Giroud ni useless
..

 Hata Mertesacker Mlimuona beki wa ovyo kwakua hachuni ngozi za watu
eti haleti ubabe hana speed hapigi tackling kumbe mnasahau kua mpira
ni mbinu tu sio kua na mambio wengi ... Dan Welbeck ana mambio kibao
manguvu mengi ila ni mwehu, januzaj hana hata nguvu ila ni super...
Muacheni Giroud afanye kile anachoweza kufanya...

 mabeki wanaopenda Kula sahani moja na washambuliaji kama koscienly
kiboko yao ni haya majitu makubwa yenye nguvu zao kama Giroud,
ibrahimoc na akina drogba kwakua wataenda kukaba alafu wanawekwa
ubavuni wanatulia then Forward Hawa wanapiga pass maeneo yale aliotoka
hao mabeki...

 ila mabeki hawa akina Koscienly wakikutana na washambuliaji
mnaowataka nyinyi wanakua wanajua sana kuwazuia... GIROUD ana deserve
Kuheshimiwa
 

No comments:

Post a Comment