Search This Blog

Wednesday, November 27, 2013

CECAFA CHALLENGE CUP 2013 KUANZA RASMI LEO, STAR v ZAMBIA…TAKWIMU ZA TIMU ZOTE

Na Baraka Mbolembole

Timu ya Taifa ya Kenya ' Harambee Stars', leo itakata ' utepe' wa
michuano ya Mataifa ya ukanda wa CECAFA, kwa kucheza na timu ya Taifa ya Ethiopia. Wenyeji hao wa michuano ya sasa na makamu bingwa wa taji hilo, wanapewa nafasi kubwa ya kuvuka kundi A, mbele ya Ethiopia,
Zanzibar, na Sudan Kusini.

Mabingwa watetezi, Uganda wao wapo kundi C, pamoja na Rwanda, Sudan, na Eritrea katika kundi linalotarajiwa kuwa gumu zaidi katika michuano hiyo. Moi Kasarani na Nyayo Stadium, ni viwanja viwili vilivyopo
katika jiji la Nairobi, Kisumu Stadium, Mombasa, na Machakos ni idadi
ya viwanja vitano ambavyo vitazipokea timu 12. Mapema leo mchana wawakilishi wengine wa Tanzania, timu ya Zanzibar Heroes itacheza na  Sudan Kusini katika mchezop wa kwanza kabisa mwaka huu.

  KILIMANJARO STARS vs ZAMBIA
Timu ya Taifa ya Tanzania Bara itaanza kibarua chake cha kwanza siku ya kesho, Alhamis kwa kucheza na timu ' alikwa' ya Zambia katika mchezop unaosubiliwa kwa hamu na wapenzi wa soka. Zambia, mabingwa wa michuano ya Mataifa ya Ukanda wa Kusini mwa Afrika, COSAFA, iliifunga Kilimanjaro Stars katika mchezo wa mwisho kukutana katika michuano hii, walipoalikwa kwa michuano iliyofanyika, Dar es Salaam, 2010.
Mbele ya Rais wa Jamhurio ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, Stars ilipoteza kwa kulala bao 1-0 siku ya ufunguzi. Disemba mwaka uliopita, Taifa Stars iliifunga timu ya Zambia kwa bao 1-0 katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki huku ' Chipolopolo' wakiwa na nyota wao waliotwaa taji la mataifa ya Afrika, februari, 2012.
  STARS, MATUMAINI YOTE KWA NGASSA
Moja kati ya silaha za hatari katika michuano hiyo ni kiungo mshambuliaji, Mrisho Ngassa. Ni mchezaji ambaye huvuta hisia kubwa za mashabiki hasa timu yake inapokuwa nje ya Tanzania, kasi, ujanja, unyumbulifu, na kucheza kwa kuhaha sehemu kubwa ya uwanja ni sifa ambazo zinampa nafasi ya kipekee kutamba katika michuano hii.
Wakati, kocha wa Stars itambidi asubiri hadi mapema mwezi ujao kupata huduma za washambuliaji wake wawili, kati ya watatu katika safu ya mashambulizi, Mbwana Samatta na Tomas Ulimwengu, ambao watakuwa na mchezo wa marejeano wa fainali ya kombe la shirikisho Afrika, wikiendi hii wakiiwakilisha klabu yao ya TP Mazembe, Kim Poulsen atamtegemea mfungaji huyo bora wa michuano iliyopita nchini Uganda.
Elius Maguli, Juma Luizio, Joseph Kimwaga, na Amri Kiemba wawili kati yao wanataraji kuanza sambamba na Ngassa katika safu ya mashambulizi. Itakuwa ni nafasi nzuri kwao na pengine kijana Said Dilunga anaweza kufanya vizuri zaidi yao kama atapewa nafasi ya kutosha.
Katika nafasi ya kiungo, KIM, bado anao wachezaji ambao wana uwezo na uzoefu wa kutosha, SAlum Abubakary atakuwa akicheza michuano yake ya pili, sambamba na Frank Domayo na wawili hao waliweza kucheza vizuri japo waliambulia nafasi ya nee baada ya kufungwa na Zanzibar katika mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu. Kwa upande wa uzoefu itakuwa ni pigo kubwa kwa Stars kama wachezaji hao vijana watashindwa kuendena na michuano kwa kigezo cha uzoefu wao mdogo. Ni vijanma ambao wameshikilia namba katika vilabu vyao vya Azam FC, na Yanga kwa zaidi ya miezi 14 sasa, na wamekuwa chaguo la kwanza katika michezo zaidi ya 15 ya Kilimanjaro Stars, na Taifa STars katika kipindi cha mwaka mmoja sasa
Wanatakiwa kujiam,ini zaidio na kuongeza uimakini katika mchezo dhidi ya Zambia, timu ambao husifika kwa kasi yao mchezoni na mchezo wa pasi za haraka haraka zile fupifupi, Kwa, Salum sina shaka ataweza kuwazima kama ilivyo kawaida yake, ni mtaalamu wa pasi fupi na ndefu, ni nadra kupoteza au kupiga pasi ' fyongo' uwanjani, wakati Domayo akisifika kwa utulivu wake, bado viongo hao wamekuwa wakisumbuliwa na tatizo la kushindwa kutengeneza nafasi za mwisho japo muda mwingine huoneka kumiliki mchezo kwa kiasi kikubwa.
Wakati, Samatta na Ulimwengu tukisubiri huduma zao silaha yetu kubwa sasa ni Ngassa, ni vipi tunaweza kumchezesha na akaisadia timu, mbio zake, akili yake na uwezo wake alionao wa kutambua afanye nini atapokuwa amefika katika lango la adui, Domayo anaweza kupiga pasi ndefu zilizotimilifu itakuwa vyema kumtumia huyu kupiga pasi za haraka kwa Ngassa. Ni wazi Zambia watamili mpira mpira hiyo ni kutokana na namna tunavyoshindwa kuwa mashindanoni. Kwa nini nasema hivyo? Wakati mwingine ni lazima tuwe wazi wachezaji wetu hutuangusha hasa pale tunapokuwa tunaweka imani kubwa juu yao.
Kufungwa michezo mitatu, kati ya sita katika michuano iliyopita ni sawa na kutoa udhibitisho huo, wakati tulipofungwa mchezo wa kwanza na Burundi, ilitukumbusha kupandisha kiwango chetu cha uchezaji, hiyo ilitusaidia hadi kuwa na wafungaji bora wawili siku ya mwisho wa michuano. Tulicheza vizuri katika michezo miwili tu iliyofuata, lakini kipigo kutoka kwa Uganda kilikuwa ni ' kizito sana' katika vichwa vya mashabiki wa soka nchini. Tulifungwa kidhaifu sana katika mchezo wa nusu fainali huku Watanzania wakiamini kuwa ilikuwa nafasi yetu kuvunja utawala wa zaidi ya miaka kumi wa Uganda kutofungwa nyumbani.
Uzoefu wa wachezaji kama Kelvin Yondan, Athumani Idd ' Chuji' , Kiemba, Ngassa, Erasto Nyoni, Ivo Mapunda, usiishie katika uwakilishi wa uwanjani tu, wanatakiwa kuwakumbusha wachezaji vijana kama kina Ramadhani Singano, Domayo, Dilunga, Kimwaga na wengine umuhimu wa kuona fahari kushinda mataji wakiwa katika jezi ya taifa. Wakati tulipopata taji la mwisho mwaka 2010 kuna vijana ambao walitoka mitaani na kupata nafasi ya kukutana na watawala wa juu wa nchini. Ni fahari kuichezea timu yako ya Taifa. Ila mafanikio ndiyo kipimo sahihi cha ubora wa jambo lolote. HIvyo wachezaji wanatakiwa kufahamu kuwa tangu kizazi na kizazi wapo wachezaji ambao wamekuwa wakiiwakilisha nchi, ila wale waliofanikiwa kushinda chochote ndiyo waliopata nafasi ya kufika bungeni, ikulu na sehemu nyingine ambazo si rahisi kufika.
 KUJIAMINI KUPITA KIASI
Japo umakini limekuwa tatizo kubwa kwa Stars, kujiamini kupitiliza imekuwa ni sumu ambayo imekuwa ikituangamiza sisi wenyewe. WAtazame, Salum, Domayo na safu ya ulinzi. JInsi wanavyokuwa wanacheza wakati tukimiliki mpira imekuwa kama hawajui umuhimu wa kutengeza nafasi za kufunga mabao. Hii ni michuano ya mtoano. Nafasi moja, bao moja, kufungwa inamaanisha kuwa mchezo ujao utakuwa ni mgumu kuliko kama mngeshinda, na nafasi inakuwa ndogo ya kusawazisha mambo.
Safu ya ulinzi, Nyoni, anatakiwa kupevuka kiuchezaji sasa na kuacha na soka la ' kipima joto', huwa hatabiriki , ingawa akiwa katika siku yake nzuri utapenda kuona anavyokuwa akiisaidia timu katika mashambulizi na kuzuia, ila akiwa hovyo utatamani apasi, akisumbuliwa mara mbili au tatu hupoteza kujiamini na umakini wake unakuwa chini zaidi. Kwa kifupi safu za ulinzi wa pembeni zikiwa imara na kufanya kazi ipasavyo hufanya ulinzi wote kuimarika, ila wakiwa katika kiwango cha kupoteza mipira hovyo na kushindwa kujiamini katika maamuzi yao hupelekea kuvuruga mambo na wakati walinzi wa kati wakishirikiana na viungo kujaribu kuweka mambo sawa mara nyingi tunajikuta tukipotea kabisa uwanjani. Wachezaji wa ulinzi watakiwa kucheza soka lililokamilika kwa wakati huu wakiwa na michezo mingi katika historia yao.
" Kama utacheza vizuri na kushinda hilo ni bora, ila kama hautocheza vizuri kwa namna yoyote ile, hakikisha ushanda kwa  namna yoyote" aliwahi kusema, Luis Aragones, kocha wa kwanza kuipa Hispania taji baada za kupita miaka zaidi ya 40.
 BURUNDI, UGANDA, ETHIOPIA
Stars itacheza tena na Burundi katika kundi la B, na matokeo yao dhidi ya ' Risasi za Shaba' hapo kesho yanaweza kuufanya mchezo dhidi ya makamu bingwa hao wa mwaka 2004 kuwa mgumu zaidi na kuamua hatma ya kundi. Mwaka jana bao lililofungwa na Suleimani Ndikumana lilizamisha Stars nchini Uganda katika mchezo wa hatua ya makundi. Burundi, sambamba na Uganda, na Ethiopia wanaitumia michuano hii ili kujiweka sawa na michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani, CHAN 2014, nchini Afrika ya Kusini, mapema mwaka ujao.

TAKWIMU
Hizi ni takwimu za kila nchi katika michuano hiyo tangu kuanzishwa.
Namba ni nafasi ambayo timu huonesha ilimazima katika nafasi gani
1' Huonesha ni nafasi ya kwanza, Namba mbili huwakilisha nafasi ya pili, Namba tatu kwa nafasi ya tatu kama ilivyo kwa namba nne kwa nafasi ya nne.

Burundi
1 –
2 2004
3 –
4 1999, 2007, 2008
Ivory Coast
1 –
2 2010[b][i]
3 –
4 –
Eritrea
1 –
2 –
3 –
4 1994
Ethiopia
1 1987, 2001, 2004, 2005
2 –
3 2000
4 1995, 2010
Kenya
1 1975, 1981, 1982, 1983, 2002
2 1979, 1985, 1991, 1999, 2001, 2008, 2012
3 1978, 1988, 1989, 1994, 1995, 2003
4 1977, 1984, 1996, 2004
Malawi[i]
1 1978, 1979, 1988
2 1975, 1984, 1989
3 1977, 1980, 1985
4 1983, 1992
Rwanda
1 1999[b]
2 2003, 2005, 2007, 2009, 2011
3 1999, 2001, 2002, 2006
4 2000, 2001[b]
Sudan
1 1980, 2006, 2007
2 1990, 1996[b]
3 1996, 2004, 2011
4 1991, 2003
Tanzania
1 1974, 1994, 2010
2 1973, 1980, 1981, 1992[b], 2002
3 1979, 1990, 2008
4 2009, 2011, 2012
Uganda
1 1973, 1976, 1977, 1989, 1990, 1992, 1996, 2000, 2003, 2008, 2009, 2011, 2012
2 1974, 1982, 1994, 1995[b], 2000
3 1983, 1984, 1987, 1991, 2007, 2010
4 1978, 1981, 1985, 2002, 2005, 2006
Zambia[i]
1 1984, 1991
2 1976, 1977, 1978, 1988, 2006
3 1981, 1992
4 1980, 1989
Zanzibar
1 1995
2 –
3 2005, 2009, 2012
4 1979, 1982, 1987, 1990
Zimbabwe[i]
1 1985
2 1983, 1987
3 1982
4 1988
By number of titles won and editions participated in Team 1ST 2ND 3RD 4TH Pld Pldlst Uganda 13 5 6 6 35 2012 Kenya 5 7 6 4 34 2012 Ethiopia 4 – 1 2 17 2012 Tanzania 3 5 3 3 33 2012 Malawi 3 3 3 2 21 2012 Sudan 3 2 3 2 19 2012 Zambia 2 5 2 2 20 2010 Zimbabwe 1 2 1 1 16 2012 Zanzibar 1 – 3 4 32 2012 Rwanda B 1 – – – 2 2001 Rwanda – 5 4 2 16 2012 Burundi – 1 – 3 13 2012 Côte d'Ivoire B – 1 – – 1 2010 Eritrea – – – 1 10 2012 Djibouti – – – – 10 2011 Kenya B – – – – 2 1994 Seychelles – – – – 2 1994 Somalia – – – – 23 2012 South Sudan – – – – 1 2012 Sudan B – – – – 1 1996 Tanzania B – – – – 1 1992 Uganda B – – – – 2 2000 Zimbabwe U23 – – – – 1 2

No comments:

Post a Comment