Search This Blog

Saturday, November 23, 2013

ADEN RAGE AHIRISHA MKUTANO WAKE NA WAANDISHI WA HABARI MPAKA KESHO

Baada ya kurejea kwa mbwembwe jana na kusisitiza yeye bado ndio mwenyekiti halali wa klabu ya Simba, Ismail Aden Rage leo aliitisha mkutano wa waandishi wa habari katika makao makuu ya klabu hiyo Kariakoo msimbazi, lakini katika hali ya kushangaza Rage ameiharisha mkutano huo.

Waandishi wa habari wakiwa tayari wanawasili msimbazi ikatoka taarifa kwamba mwenyekiti huyo aliyesimamishwa na kamati ya utendaji mapema wiki hii hatoweza kukutana leo kwa kuwa anaenda kukutana na uongozi wa TFF na kwahiyo mkutano wake na waandishi wa habari atafanya kesho Jumapili.

Msemaji wa klabu hiyo Ezekiel Kimwaga muda mfupi uliopita kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Facebook alitoa taarifa rasmi juu ya kuhairishwa kwa mkutano huo mpaka kesho.

No comments:

Post a Comment