Search This Blog

Thursday, October 17, 2013

PUMA YASITISHA MARA MOJA UDHAMINI WA SAFA.

Kashfa za upangaji matokeo zilizokuwa zikikikabili chama cha soka cha nchini Afrika Kusini ( SAFA ) zimepelekea kampuni ya PUMA iliyokuwa inazivalisha timu za Taifa za nchi hiyo  kusitisha mkataba mara moja.
Taarifa za PUMA kusitisha mkataba na SAFA zimekuja siku mbili baada ya benki ya Absa nayo kusitisha mkataba uliodumu kwa kipindi cha miaka 6.
Mnamo mwezi Disemba, uchunguzi wa Fifa ulibaini upangwaji wa matokeo kwenye baadhi ya michezo ya kujipima nguvu iliyoihusu Bafana Bafana wakati wa maandalizi ya fainali za kombe la dunia za mwaka 2010.
Kashfa hizo zilipelekea kusimamishwa kwa aliyekuwa raisi wa SAFA Kirsten Nematandani.

No comments:

Post a Comment