Search This Blog

Monday, October 28, 2013

MAJERUHI SIMBA HADI MWEZI UJAO


Viungo wawili chipukizi wa timu ya soka ya Simba, Abdallah Seseme na Ibrahim Twaha wataendelea kuuguza majeraha yao hadi baadae mwezi ujao. Seseme bado anauguza majeraha ya kuvunjika vidole viwili vya mwisho, wakati Twaha aliyesajiliwa msimu huu akitokea timu ya Coastal Union anasumbuliwa na maumivu ya nyama za paja.
Wakisema hayo kwa nyakati tofauti wakati walipozungumza na mtandao huu viungo hao wamekiri kuwa hawana nafasi ya kurejea tena uwanjani katika michezo ya mzunguko wa kwanza.
" Niliumia vidole viwili vya mwisho vya mguu wa kushoto wakati wa mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Lipuli. Mguu ulikleki sasa nimewekewa P.O.P hadi mweizi ujao. Nina miezi miwili sasa bado nauguza majeraha haya" anasema Seseme
Kwa sasa nipo katika uchunguzi kama nimechanikla au ni maumivu ya kawaida tu. Nimeumia nyama za paja la mguu wa kulia" anasema Twaha ambaye amecheza michezo mitatu ya timu yake huku akikosa michezo miwili ya mwanzo ya msimu huu kwa kuwa timu yake ya zamani ilimuwekea pingamizi.
Simba itacheza na timu ya Azam FC katika mchezo wa raundi ya 11 ya ligi kuu wakijaribu kutanua wigo la pointi katika kilele cha msimamo.

No comments:

Post a Comment