Search This Blog

Friday, October 4, 2013

HATIMAYE MECHI ZA LIGI KUU KUONYESHWA TBC 1

Azam Media Limited imefanikiwa kukamilisha utaratibu wa ushirikiano na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) utakaowawezesha mashabiki wa kandanda kote nchini kunufaika kwa kuona michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom kila mwishoni mwa juma hadi kukamilika kwa nusu ya msimu wa 2013/14 kupitia TBC1 kwa hisani ya AzamTV.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Bodi ya Ligi (Kamati ya Ligi) wameeleza kuunga mkono utaratibu huu makini.

“Baada ya kupata haki za matangazo ya luninga ya Ligi Kuu ya Vodacom, moja ya shabaha zetu kuu imekuwa ni kuhakikisha kuwa tunafanikiwa kurusha matangazo yanayokidhi viwango vya kimataifa kwa ubora. Ili kufanikisha shabaha hiyo tumewekeza vilivyo katika teknolojia ya kisasa ya vifaa vya matangazo ya nje (Outside Broadcasting) na katika mafunzo kwa watumiaji wa vifaa hivyo. Ninayo furaha kusema kuwa matayarisho yamekwenda vema kiasi kwamba tumejikuta tuko tayari kurusha matangazo ya kiwango cha juu kabla hata ya kuzinduliwa kwa huduma kamili za AzamTV”, alisema Rhys Torrington, Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media Limited.



“Kwa kuwa mashabiki wengi kote nchini wanangojea kwa hamu kubwa kuziona timu wazipendazo, imeonekana ni vema kuanza kuonesha michezo hii ya Ligi sasa. Kwa kuzingatia hali hiyo, nilifanya mazungumzo na rafiki zetu pale TBC na kuwaomba iwapo wana uwezo na kuridhia kurusha matangazo yetu ya moja kwa moja bila ya malipo yoyote kuanzia mwisho wa juma hili hadi kukamilika kwa nusu msimu. Tulifanikiwa kufikia makubaliano kwa haraka na sasa tunafanyia kazi masuala ya kiufundi yatakayowezesha kuwa tayari kwa ajili ya mchezo wa Jumamosi utakaofanyika Uwanja wa Taifa”, Aliongeza Bw. Torrington.

Mara tu huduma kamili za AzamTV zitakapozinduliwa majuma machache yajayo, matangazo ya michezo ya Ligi Kuu kwa wigo mpana yatakuwepo pia kwenye chaneli yake hadi mapumziko ya nusu msimu. Baada ya hapo matangazo ya Ligi Kuu ya Vodacom yatapatikana kwa wale tu watakaokuwa na visimbuzi (decorders) vya AzamTV.

3 comments:

  1. Dah! Afadhali maanake nimesubiria saana kuona huu uondo na utam wa soka la bongo, bila shaka itakuwa mwisho wa kuonewa kwa club zote ukiwaondoa hawa wababe juu ya waamuzi wasiofuata sheria za mpira.
    Pia ni fursa tosha kwa vilabu na wachezaji.
    Angalizo kwa vile match zitarushwa live, wachezaji waelimishe zaid juu ya nidham na kuwajibika zaid

    ReplyDelete
  2. Dah! Afadhali maanake nimesubiria saana kuona huu uondo na utam wa soka la bongo, bila shaka itakuwa mwisho wa kuonewa kwa club zote ukiwaondoa hawa wababe juu ya waamuzi wasiofuata sheria za mpira.
    Pia ni fursa tosha kwa vilabu na wachezaji.
    Angalizo kwa vile match zitarushwa live, wachezaji waelimishe zaid juu ya nidham na kuwajibika zaid

    ReplyDelete
  3. Dah! Afadhali maanake nimesubiria saana kuona huu uondo na utam wa soka la bongo, bila shaka itakuwa mwisho wa kuonewa kwa club zote ukiwaondoa hawa wababe juu ya waamuzi wasiofuata sheria za mpira.
    Pia ni fursa tosha kwa vilabu na wachezaji.
    Angalizo kwa vile match zitarushwa live, wachezaji waelimishe zaid juu ya nidham na kuwajibika zaid

    ReplyDelete