Search This Blog

Friday, October 18, 2013

COUNTDOWN DAR DERBY: NAIPENDA SIMBA, SHABIKI WA YANGA NA BARAKA MBOLEMBOLE



 Baraka Mbolembole 
Vinara wa ligi kuu Tanzania Bara, Simba SC watakuwa uwanjani siku ya jumapili ijayo katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwakabili mabingwa watetezi na mahasimu wao wa soka nchini Yanga SC, katika mchezo wa raundi ya tisa. Timu zote zinatumia uwanja wa Taifa kama uwanja wao wa nyumbani, ila katika mchezo ujao Yanga watakuwa wageni, na Simba watakuwa timu mwenyeji.
Simba wapo juu ya Yanga kwa tofauiti ya pointi tatu, na wanaweza kuongeza pengo hadi kufikia tofauti ya pointi sita ebdapo watapata ushindi. Katika michezo nane iliyopita, Simba imekusanya pointi 18, huku wapinzani wao wakiwa na pointi 15 katika nafasi ya nne ya msimamo.
         ZILIPOTOKA
Simba iliifuinga timu ya Tanzania Prisons wiki iliyopita kwa bao 1-0, wakati mahasimu wao Yanga walipata ushindi wa ugenini dhidi ya Kagera Sugar, mjini Bukoba waliposhinda kwa mabao 2-1.
          OKTOBA 20
Yanga wanapewa nafasi kubwa ya ushindi katika mchezo huo kwa kulinganisha aina ya wachezaji wa pande zote mbili na kuwachambua katika makaratasi. Kwa ubora wa mtazamo Yanga wnaoneka kuwa na pointi katika hili, kwa kuwa wamekuanya wachezaji ' wa bei mbaya' katika kikosi chao ukilinganisha na wale wa Simba. Lakini hiko si kigezo sahihi cha kuwapa ' pointi' mbele ya Simba, ukizingatia tayari walionja radha ya kichapo waluipocheza na Azam FC, huku Simba wakifanya vizuri na kuwa timu ambayo haijapoteza mchezo wowote hadi sasa.
        MBINU ZA MCHEZO
Mara zote Simba wamekuwa watala wa eneo la katikati ya uwanja, pindi wakicheza na Yanga. Wana wachezaji ambao wanaweza kucheza katika mfumo wa 4-4-2, au ule wa 4-3-3 kwa usahihi, mifumo hii imekuwa ni mizuri kwao katika michezo ya ' DAR- PACHA' kwa kipindi kirefu sasa. Ila kuelekea mchezo wa jumapili hii inaonekana kuna hatari ya timu hiyo ' kupotea' mchezoni na kutoa utawala kwa timu ya Yanga ambayo pia inauwezo wa kusoma mifumo ya timu pinzani na kuivuruga wakitumia wachezaji wao wa ' kazi'
Kocha wa Simba, Abdallah Kibadeni kwa wiki nzima amekuwa akijinasibu kwa atashinda, wakati yule wa Yanga, Ernest Brandts amekuwa bize kuhakikisha wachezaji wao wanaongeza kiwango chao cha uchezaji, umakini, na nidhamu. Kumekuwa na tetesi kuwa makocha Kibadeni na msaidizi wake Jamhuri Kiwelo, kuingia katika tofauti na baadhi ya wachezaji wa timu yao.
Ila sikupendezwa na namna alivyokuwa bize kuongelea mambo hayo nje ya timu, makocha hao hawakujali ni sehemu gani nzuri ya kukaa na kuzungumzia mambo yao ya ndani, ilikuwa ni kazi ya msemaji wao Ezekiel Kamwaga kukanusha au kukubali kuhusiana na habari za kuwepo kwa ugomvi kati ya kocha na baadhi ya wachezaji muhimu. Wakati muda umekaribia kufika na kila kitu kuwa hadharani, makocha hao watakuwa wakikuna vichwa na kutazama ni namna gani wanaweza kuleta ' heshima'.
Nassoro Masoud, Issa Rashid hawa watakuwa walinzi wa pembeni wa Simba katika mchezo huo, japo anaweza kuingia Haruna Shamte upande wa kushoto kama, Kibadeni ataamua kucheza kamari ili kujaribu kuwadhibiti washambuliaji wa pembeni wa Yanga, Mrisho Ngassa na Saimon Msuva.
Yanga wana kawaida yao ya kuimaliza mechi yoyote ngumu wakitokea pembeni ya uwanja, Ngassa ni mchezaji mjanja, mnyumbulifu, ana kasi, chenga, na maarifa ya kufunga ama kutoa pasi, na uwepo wa Msuva upande mwingine wa uwanja naona kabisa kulikuwepo na fasi ya Henrry Joseph katika eneo la kiungo la Simba. Jonas Mkude ni kiungo mzuri sikatai ila bado ana mengi ya kujifunza ili kuingia katika kundi la viungo bora nchini, ana shambulia vizuri, ndiyo maana tayari ana mabao matatu katika michezo saba aliyocheza, ila si mzuri katika kucheza mipita ya ' tackling' . Hivyo uwepo wa Joseph ambaye ni mzuri katika vyote hivyo vingeweza kumfanya Mkude kuwa na nguvu ya kuisukuma timu mbele na ,kuicheza huku wakiwa na jukumu la kuwasaidia walinzi wao wa pembeni wakati wakiwa wanashambuliwa.
Mtu, mwingine muhimu kwa Simba katika eneo hili la kati ni Amri Kiemba, alicheza vibaya katika mchezo wa mwisho wa watano hao wa jadi, Mei 18, mwaka huu na katika siku za karibuni amekuwa akionesha kiwango cha chini. Kiemba amecheza michezo nane ya timu yake na hajafunga bao lolote kitu ambacho kilimfanya kocha wake kumuweka benchi katika mchezo uliopita. Ila anaweza kucheza vizuri siku ya jumapili na kuisadia Simba kwa kuwa Simba hadi sasa haina mbadala wa nafasi yake. Mechi ambazo Kiemba ameshindwa kuongoza eneo la kiungo Simba ilibaki ikimtegemea Haruna Chanongo, na hapo wakawa wanacheza na kutegemea upande wao wa kulia ili kupata mabao, bila shaka Chanongo anaweza kumsumbua mlinzi wa kushoto wa  Yanga David Luhende ila na wasiwasi kuwa anaweza kutumia muda mwingi kumsadia Chollo ili kumzima Ngassa, kama Yanga wataongoza mchezo.
Kiemba, anauwezo wa kukaa na mpira na kupiga pasi nzuri za mwisho huku rekodi yake ya ufungaji ikiwa ni nzuri pia Simba inaweza kunufaika na vitu alivyo navyo na kujaribu kuwazima ' viungo- wahamasishaji' Athuman Idd ' Chiji' na Haruna Niyonzima, ambao waliweza kutawa eneo la katikati. Yanga hawana safu kali sana ya mashambulizi, ila wana washambuliaji wa ' mechi kubwa', Hamis Kizza na Didier Kavumbagu wanaweza kuwaumiza kwa mara nyingi Simba endapo watarusu krosi, na pasi za kunyeza, sina shaka na uwezo wa Joseph Owino, huyu ni mlinzi kiongozi wa wenzake mchezo, ila uwepo wa washambuliaji wenye kariba ya Kizza na Kavu, utakuwa mtihani mkubwa kwao. Wanaweza kuibuka muda wowote mchezo na kuimaliza mechi kama walivyofanya Mei 18
Amis Tambwe, Chanongo kwa pamoja wamefunga mabao 11 katika michezo nane iliyopita, mabao manne pungufu yaliyofungwa na timu ya Yanga. Tambwe amekua akinufaika na uwepo wa Bertam Mombeki ambaye amekuwa akiwapa wakati mgumu walinzi wa timu pinzani, Mombeki hutumia umbo lake kumiliki kila mpira unaopigwa katika eneo lao, ni mzuri kwa mipira ya chini na ni hatari zaidi kwa ile ya juu, Tambwe yeye amekuwa ni bingwa wa kukaa katika maeneo ya hatari na kutumia kila nafasi anayoipata kwa umakini mkubwa, ni mzuri katika mipira ya ' kuunganisha', ana jua ni wapi goli lilipo, ila mara zote hutegemea timu yake kucheza na kuongoza mchezo. Endapo Simba watamili mchezo Tambwe atafunga mara mbili, kwa kuwa sijaona bado ubora wa sasa wa Nadir Haroub na Kelvin Yondan, bado wapo katika kujiweka sawa na wamekuwa wakipoteana mara kwa mara, ila Mbuyu Twite anaweza kuwasaidia kwa kuwasogeza Simba nyuma ili kuwafanya wawe bize na kukaba.
   NANI MSHINDI

Abel Dhaira na Ally Mustapha wote wameonesha udhaifu katika maeneo yao, Dhaira amefungwa mabao matano na Mustapha amefungwa nane. Kushina au kufungwa kwa timu zao kutagemea na kikla mmoja kupandisha kiwango chake cha uchezaji wa mipira iliyokufa, ushapu wa kuzungumza na kuitokea mipira. Atayayekuwa anatematema sana bila shaka ataimamiha timu yake. Naipenda Simba, Shabiki wa Yanga.....Dakika tisini za kukumbwa ' Mimi naikumbuka ile ya marehemu Mutesa, akiaina fulani ya muziki katika moja ya kona za uwanja wa Taifa huku akionesha ishara ya mkono juu'

   0714 08 43 08

1 comment: