Search This Blog

Saturday, September 7, 2013

THIAGO SILVA: NILIIKATAA BARCELONA BAADA YA KUONA WALIVYOMFANYIA ABIDAL

Mlinzi wa PSG Thiago Silva amekiri alikataa kujiunga na Barcelona wakati wa dirisha la usajili lilopita kwa sababu ya namna walivyomfanyia beki wa kushoto wa timu hiyo Eric Abidal.

Abidal aliachwa na Barca mara baada ya msimu kuisha na hivyo akaenda kujiunga na AS Monaco.
Thiago Silva akiongea na El'equippe alisema: "Kuna vitu vilitokea kwa bahati mbaya ay nzuri vikanifanya nisiendelee na mazungumzo ya kuhamia Barca. 
"Halikuwa jambo zuri kwangu na familia yangu. Ilikuwa ni ndoto yangu kuvaa jezi ya Barcelona, lakini haikuweza kutokea.
"Tangu ilipoamuliwa kwamba ningebaki PSG, nilivaa jezi yangu na nina furaha sana kuwa hapa kuisadia timu yangu. 
"Niliona namna ilivyokuwa kwenye suala la Abidal na sikupenda walichomfanyia. Hawakuwa sawa - hawakutunza na kuitimiza ahadi yao kwa Abidal ambaye ni mtu mzuri na hawakufanya lolote kumsaidia wakati alipotoka kwenye matatizo."

No comments:

Post a Comment