Search This Blog

Saturday, September 7, 2013

TAIFA STARS YAPIGWA 2-0 NA GAMBIA KATIKA KUHITIMISHA KUSHINDWA KWAO KWENDA BRAZIL 2014

Timu ya taifa ya Gambia inayoshika mkiani mwa kundi la C kwenye michuano ya kugombea nafasi ya kushiriki michuano ijayo ya kombe la dunia imemaliza mbio hizo kwa ushindi wa kulinda heshima dhidi ya timu ya taifa ya Tanzania kwa kushinda 2-0 katika uliomalizika hivi punde huko Gambia.
 

Kiungo Mustapha Jarjue alifunga mabao yote mawili katika mchezo huo - kila kipindi akifunga bao moja.

Jarjue aliiweka mbele Gambia kwa bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza dakika za mwisho kabla ya kuongeza la pili dakika 6 baada ya mapumziko.

Pamoja na ushindi lakini Gambia imeshindwa kuiondoa Tanzania katika nafasi ya 3 ya kundi hilo baada ya kumaliza nafasi ya nne - wakiwa na pointi sita kutoka michezo sita iliyopita ya kundi hilo.
Cote d'Ivoire wamemaliza wakiwa juu ya kudni hilo wakiongoza kwa pointi 13 huku wakielekea kwenye mchezo wa mwisho wa kukamilisha ratiba dhidi ya Morocco.

2 comments:

  1. Ndicho tulichopanda tujipange kwa michuano ijayo

    ReplyDelete
  2. wa hapa hapa hao..........

    ReplyDelete