Search This Blog

Tuesday, September 24, 2013

MAONI YA SHABIKI WA MAN UNITED: MOYES ASIRUDIE MAKOSA AU TUJIANDAE NA AIBU YA KUKOSA CHAMPIONS LEAGUE MSIMU UJAO

Nilinyanyuka kwenye kochi la nyumbani kwangu nikiwa mzito na kwenda kulala moja kwa moja ikiwa ni mapema sana kuliko kawaida yangu. Hii ilikuwa baada ya kuangalia timu yangu niipendayo ikadhalilishwa katika dimba la Etihad usiku wa jumapili ya wiki iliyopita. Nilijiuliza swali moja tu hivi ni kweli hata kuna ushindani mkubwa msimu huu kama inavyosemekana baina ya vilabu viwili vya jiji la Manchester.

Vilabu vyote viwili vinajinasibu kwamba vipo katika muda wa mapito baada ya kubadilisha makocha, lakini ushindi wa 4-1 wa City dhidi ya majirani zao ulionyesha utofauti mkubwa uliopo baina ya vikosi vya klabu hizi mbili.

City wana ukamilifu kwenye idara, ubora wa ufundi, na matamanio ya dhati ya kurudisha ubingwa wa Premier League chini ya kocha mwenye ufundi mkubwa hasa kwenye mechi kubwa kama hizi. 


MSIMAMO WA PREMIER LEAGUE 
TIMU

1. Arsenal
2. Tottenham
3. Man City
4. Chelsea
......................
5. Liverpool
6. Everton
7. Southampton
8. Man Utd

MECHI
5
5
5
5
........
5
5
5
5

GD

5
4
8
4
........
2
2
1
1
Points

12
12
10
10
........
10
9
8
7
Katika michezo mitano ya ligi ambayo tayari Man United tumeshacheza, inaonekana wazi inabidi tubadilike sana au tusihau kuhusu ubingwa na kuweka kipaumbele katika kumaliza ndani ya TOP 4.

David Moyes alipewa ratiba ngumu - na hata akalalamika kuhusu ratiba hiyo ngumu - lakini mscotish huyu amepata pointi moja tu katika michezo yote mitatu tuliyocheza na timu kubwa zenye upinzani nasi katika ligi na kikosi chake kimecheza kwa kiwango cha kuridhisha kwenye mchezo mmoja tu wa ligi. 


Ukiachana na mchezo wa kufungua ligi dhidi ya Swansea, United tumekuwa tukionekana kukosa ubora wa pamoja kama timu, huku safu yetu ya ulinzi ikiyumba hasa kwa viwango vya wachezaji wetu wenye umri mkubwa kiasi kama Rio Ferdinand na Patrice Evra.

Ujio wa Marouane Fellaini katika siku ya mwisho ya usajili ulikuwa muhimu sana, lakini United bado wana tatizo sana katika safu ya kiungo - hawana uimara wa kuweza kufananisha na safu ya kiungo cha Chelsea, City, Tottenham, na sasa hata Arsenal wanaoringia ujio wa 'The Master of Assists' Mesut Ozil na mkabaji Matheiu Flamini.

Kitu kingine cha kuhuzunisha ni upangaji wa kikosi wa kocha, inaonekana bado anafanya majaribio wakati wapinzani wetu wengine wanaogombea TOP 4 wakiwa wameanza vizuri ligi, pamoja na kwamba wamebadilisha makocha na wengine hata wakiwa wameuza wachezaji mategemeo katika msimu uliopita.

United sasa kwa bahati nzuri tuna mechi ambazo angalau unaweza kuziita nyepesi mpaka pale tutakapokutana na 'The inform Gunners'  Arsenal November 10. Lakini angalau hizi mechi na timu ndogo tusifanye makosa au Moyes ajiandae kutuletea aibu ya kukosa ubingwa na kukosa hata kushiriki Champions League msimu unaokuja.

9 comments:

  1. in the world there are twp teams only, one is MANCHESTER UNITED and the other is OTHERS, huyu anayempangia Moyes kikosi apange kwanza cha timu yake LOCAL na NATIONAL then afuate UNITED. wanajua wanachofanya na cc tutulie tu maana hatuna mchango wowote kwenye timu zaidi ya kupiga kelele inaposhinda na kushindwa, SAF hawezi kuwa kocha maisha yote, as doesd MAN UTD haiwezi kuwa bingwa miaka yote, times change and now its our time the transition is with us!

    ReplyDelete
  2. alex alipigwa 6 na city mbona mlikaa kimya liverpool iliifunga utd 4 tena old traford mbona hamkusema mwachen jamaa afanye kaz ndo maana simba yanga kila siku mnatimua makocha

    ReplyDelete
  3. yan pale mcmu huu atachukua ubingwa ashle young kwa kujiangusha ila nyie wengine msubili mcmu ujao hata kombe la ligi hata la Fa hakuna kitu mcmu huu tim yetu ya man city iko imara alifungwa faghason 6 sembuse moyes tena siku ile ilibidi tupige hata 9 bas zeko aloizingua tukiamua tunawauzia

    ReplyDelete
  4. Ozil ndo jibu pia Van Persie maujuz aliyopewa na Prof Wenger yanaelekea kwisha.
    msisahau Van Persie alikuwa winga yule Prof wenger nimjuzi sana.

    ReplyDelete
  5. mbona SAF alipigwa 6 - 2 tena nyumbani na nimzoefu wa ligi hiyo tena sana kwa iyo ni suala la kumpa mda Moyes maana bado hajui jinsi ya kupambana na Derby kama izo ila kama ataitaji matokeo kama hayo na kuishia nafasi za Uropa ligi kwenye msimamo aendelee kuwapiga bench Nani,Kagawa Chicharito(kijana alie jaa magoli miguuni kwake) ila akiendeleza uingereza wake wa kumpanga Welbeck,Young na Valencia(sio mwingereza) wataumia na leo wanakutana na Liverpool ya Suarez, mimi nasubiri soka tu.

    ReplyDelete
  6. i support u n kwel hatuwez kuwa mabingwa sku zote coz kila m2 anataka ubingwa but tusmlaum coz msimu bado mkubwa kumbuka alikokuwa arsenal mwaka jana na wakamaliza wa tano xo big up Moyes

    ReplyDelete
  7. bado unamtazamo wa jicho moja kaka

    ReplyDelete