Search This Blog

Saturday, September 28, 2013

LIVE MATCH CENTRE: VPL - YANGA SC 1 - 0 RUVU SHOOTING


Dk 90+3 FULL TIME! Yanga 1-0 Ruvu 

Dk 89 Kiiza anachezewa faulo nje kidogo ya lango la Ruvu. Twite anapiga faulo na Ruvu wanaokoa. 

Dk 86 SUB: Yanga imefanya mabadiliko ametoka Msuva ameingia Niza Khalfan. 

Dk 78 YELLOW CARD..! Suzan wa Ruvu anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kubishana na mwamuzi. Yanga 1-0 Ruvu 

Dk 68 SUB: Ruvu wanafanya mabadiliko ametoka Ayoub Kitala ameingia Said Madega. 

Dk 65 Yanga wamebadilika na kumiliki mpira kwa kiasi kikubwa hasa baada ya kuingia Chuji. 

DDk 62 GOOOOO.....! Kiiza anaipatia Yanga bao la kwanza kwa tik-tak safi akiunganisha krosi safi ya Mrisho Ngassa. Yanga 1-0 Ruvu 

Dk 55 Lewis wa Ruvu anaumia baada ya kugongana na Mbuyu Twite. 

Dk 50 SUB: Yanga inafanya mabadiliko anatoka Domayo anaingia Athuman Idd Chuji. 

Dk 46 Elius Maguli wa Ruvu anakosa bao la wazi katika lango la Yanga mpira wa kichwa anaopiga unatoka nje. 

Yanga 0 - 0 Ruvu Shooting

Dk 45 KIPINDI CHA PILI KIMEANZA! 

Dk 45 HALF TIME! Yanga 0-0 Ruvu 

Dk 44 YELLOW CARD..! Ayoub Kitala wa Ruvu anaonyeshwa kadi ya njano kwa kumlalamikia mwamuzi kupita kiasi baada ya Suzan kumchezea rafu Kavumbagu. 

Dk 40 Jerome Lambele wa Ruvu anapiga shuti kali langoni kwa Yanga lakini mpira unatoka nje. Yanga 0-0 Ruvu

Dk 38 Kiiza wa Yanga anakosa bao la wazi akiwa amebaki na kipa wa Ruvu Abdul Seif. 

Dk 37 Yanga inapata kona lakini Ruvu wanaokoa. 

Dk 32 YELLOW CARD....! Kipa wa Yanga Ali Mustapha anaonyeshwa kadi ya njano kwa kuchelewa kuanza mpira. 

Dk 31 Niyonzima anamchezea rafu Cosmas Lewis wa Ruvu. Yanga bado hawaelewani. 

Dk 27 Yanga wamepoteana hawana mipango kama ya siku zote, lakini Ruvu wanashindwa kutumia udhaifu huo wa Yanga. 

Dk 21 Kavumbagu anakosa bao la wazi akishindwa kuunganisha krosi ya Simon Msuva. 

Dk 19 Niyonzima anaushika mpira alioanzishiwa na Ali Mustapha na Ruvu wanapata kona baada ya David Luhende kuutoa nje mpira. Yanga 0-0 Ruvu 

Dk 14 YELLOW CARD...! George Michael wa Ruvu anaonyeshwa kadi ya njano kwa kumsukuma Kavumbagu wa Yanga. 

Dk 11 Haruna Niyonzima anakosa bao la wazi akiwa ndani ya eneo la hatari la Ruvu kwa kushindwa kupiga mpira kwenye lango la Ruvu.  

Dk 6 Ruvu wanapata kona baada ya Cannavaro kuutoa nje mpira. Yanga wanaokoa kona hiyo. 

Dk 4 Yanga inapata kona baada ya Shaban Suzan kuutoa nje mpira. Kona inapigwa na Ruvu wanaokoa. 

Dk 1 Jerome Lambele wa Ruvu anamchezea rafu Haruna Niyonzima. 

Mpira ndio umeanza hapa uwanja wa Taifa kati ya Young Africans Vs Ruvu Shooting

KIKOSI CHA RUVU 
 Abdul Seif, Michael Pius, Stephano Mwasyika, George Michael, Shaban Suzan, Gidion David, Ayoub Kitala, Hassan Dilunga, Cosmas Lewis, Elius Maguli na Jerome Lambele. Sub: Godhar Misweko, Said Madega, Mangasin Mbonosi, Mau Bofu, Kulwa Mfaume, Said Dilunga na Juma Seif 'Kijiko'.

KIKOSI CHA YANGA KINACHOANZA LEO

1.Ally Mustapha 'Barthez' - 1
2.Mbuyu Twite - 6
3.David Luhende - 3
4.Kelvin Yondani 'Cotton' - 5
5.Nadir Haroub 'Cannavaro' - 23
6.Frank Domayo 'Chumvi' - 18
7.Saimon Msuva - 27
8.Haruna Niyonzima - 8
9.Didier Kavumbagu - 7
10.Hamis Kiiza 'Diego'- 20
11.Mrisho Ngassa - 17


Subs:
1.Deogratius Munishi 'Dida' - 30
2.Juma Abdul - 12
3.Oscar Joshua - 4
4.Athuman Idd 'Chuji ' - 24
5.Nizar Khalfani - 16
6.Said Bahanuzi - 11
7.Jerson Tegete - 10

1 comment:

  1. kwan shafii hiyo line up ya ruvu ungepanga kama ya yanga ungepungukiwa nini? mana hatujui sub wakina nani hat number zao hatuzijui,BE FARE KAKA AU NDIO UNAZI WENYEWE?

    ReplyDelete