Search This Blog

Friday, September 6, 2013

HATIMAYE CEO WA MAN UNITED AKIRI KUFANYA MADUDU KWENYE USAJILI

Ryan Giggs, Group Managing Director Richard Arnold, CEO Ed Woodward and Club Secretary John Alexander honours King Bhumibol of Thailand at Siriraj HospitalHatimaye baada kusemwa sana CEO wa Manchester United Ed Woodward amekiri kwamba hajafanya kazi nzuri kwa mabingwa hao katika dirisha la usajili liloisha hivi karibuni.

David Moyes, kocha mpya wa United, alitaka kuwasajili viungo wawili na beki wa kushoto wa kusaidiana na  Patrice Evra.
Lakini usajili pekee wa maana uliofanywa Old Trafford ni wa Maroune Fellaini - aliyenunuliwa dakika ya mwisho kabla ya dirisha la usajili halijafungwa kwa ada ya uhamisho wa  £27.5million.
Na Woodward ameripotiwa kutambua kushindwa kwake kuwaleta wachezaji wa waliotakiwa na Moyes - kumemfelisha.
United walishindwa katika majaribio yao ya kuwasajili  Cesc Fabregas, ambaye alichagua kubaki Barcelona, Thiago Alcantara, aliondoka Barca kujiunga na Bayern Munich, Ander Herrera wa Athletic Bilbao na kiungo wa Roma  Daniele De Rossi.
 
Pia United walishindwa katika jaribio lao la kumsaini beki wa kushoto wa Everton Leighton Baines na mkopo wa Fabio Coentrao ukashindikana. 

 


No comments:

Post a Comment