Search This Blog

Friday, September 6, 2013

ABIDAL: BARCELONA HAWAKUNILIPA HATA SENTI TANO MIEZI YOTE NILIYOKUWA NAUMWA

Eric Abidal amekasirishwa na namna maisha yake ya soka ndani ya Barcelona yalivyoisha na kusema kwamba hakulipwa chochote na klabu hiyo wakati wote alipokuwa akiugua.

Beki huyo mwenye miaka 34 alifanyiwa upasuaji wa kuwekewa ini jipya mnamo mwezi April mwaka jana, kumfanya akose michuano ya Euro na kumuweka nje ya soka kwa muda wa mwaka mmoja. Airudi kuichezea Barcelona kwenye mechi kadhaa kabla ya kuondokakujiunga na Monaco.
"Tatizo lilikuwa kwamba mkataba wangu ulikuwa unaenda mwishoni. Kwa maana hiyo ilikuwa aidha niongeze au uishe. Nilijiandaa kwa vyote," Abidal alisema katika interview aliyofanya na sports daily L'Equipe ya leo Ijumaa. "Ilikuwa ni vigumu kukubali lakini siku na jinsi. Maisha yangu ndani ya Barcelona yalikuwa yamefikia mwisho, lakini nina furaha nimeanza maisha mapya na Monaco."
Lakini Abidal amesema alikerwa na kusikitishwa namna kuondoka kwake kulivyotangazwa.
"Kitu kigumu kuelewa kilikuwa walichosema Barcelona katika mkutano wangu wa mwisho wa waandishi wa habari. Kwa kusema uamuzi ule ulitokana na sababu za kiuledi zaidi, ulivifanya vilabu vingine viwe na mashaka," Abidal alisema. "Haikuwa hata suala la fedha. Na ushahidi upo wazi kwamba miezi yote niliyokuwa kitandani naumwa, klabu haikunilipa chochote. Sasa nina bahati Monaco wameniamini - Kocha na Raisi wote wana imani juu yangu."
Abidal amecheza kwa dakika 90 katika kila mchezo wa ligi na  anategemewa kuichezea Ufaransa katika mechi ya kugombea nafasi za kucheza kombe la dunia dhidi yat Georgia.

No comments:

Post a Comment