Search This Blog

Saturday, August 24, 2013

ROBERT LEWANDOSKI: "KWANINI NILIKATAA KUJIUNGA NA MAN UNITED, REAL MADRID NA CHELSEA.'


On target: Lewandowski scored the winner for Dortmund in a 1-0 victory over Werder Bremen on Friday night


Mshambuliaji wa Borussia Dortmund Robert Lewandowski amefunguka na kusema kwamba amekataa kujiunga na vilabu vya  Manchester United, Chelsea na Real Madrid ili aendelee kucheza kwenye Bundesliga.
Baada ya tetesi za usajili kumhusisha na vilabu kadhaa barani ulaya, ikiwemo klabu hasimu ya Dortmund - Bayern Munich, Lewandowski sasa amesuluhisha tofauti zake na Dortmund na ameripotiwa kwamba tayari ameongezea marat tatu mshahara wake.a

Na mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 25 amezungumza na kusema alifuatwa na vilabu kadhaa, pamoja kuzungumza binafsi na kocha Jose Mourinho.

Baada ya kufunga mabao manne katika mchezo dhidi ya Real Madrid katika mchezo wa raundi ya kwanza wa nusu fainali ya Champions League, Mpoland huyo alipokea ujumbe wa simu kutoka Mourinho: 'Nataka uungane nami katika klabu yoyote nitakayoenda.'
Lewandowski aliiambia The Sun: 'Naweza kuthibitisha kwamba niliongea na Mourinho. Tulikuwa na mazungumzo mara kadhaa huko nyuma. Nina namba yake ya simu kwenye simu yangu. Ninahisi fahari kuwa kocha mwenye jina kubwa kama lake kunihitaji.
'Mwaka mmoja uliopita niliongea na Sir Alex Ferguson na kwa kweli lilikuwa jambo kubwa na muhimu kwangu.
Quadruple: Lewandowski scored four against Real Madrid in the first leg of the Champions League semi-finals



'Kustaafu kwa Sir Alex hakukubadilisha maamuzi yangu ya kutokwenda England. Aliongea nami mwaka mmoja uliopita, lakini haukuwa muda sahihi kuondoka. 

'Premier League ni kubwa sana, kama ilivyo La Liga. Lakini  Bundesliga ni kila kitu cha kuifanya kutawala kwa miaka mitano ijayo.'
Lewandowski pia alithibitisha kwamba alikutana na raisi wa Real Madrid Florentino Perez kwenye dimba la uwanja wa Bernabeu muda mfupi baada ya Dortmund kuweza kufuzu kucheza fainali ya Champions League.

No comments:

Post a Comment