Search This Blog

Sunday, August 18, 2013

ARSENAL NDIO MABINGWA WA SERENGETI FIESTA SOKA BONANZA NDANI YA KIGOMA

MABINGWA WA SERENGETI FIESTA SOKA BONANZA

Nahodha wa timu ya mashabiki wa Arsenal mkoani Kigoma Samweli Balina akipokea kombe la ushindi na kitita cha fedha taslimu laki tatu kutoka kwa Mkurugenzi wa Utafiti wa Clouds Media Group Bw. Ruge Mutahaba baada ya kuibuka washindi katika bonanza la Serengeti Fiesta Soccer Bonanza lililofanyika siku ya ijumaa jioni katika uwanja wa Kawawa uliopo Ujiji,  anayeshuhudia kulia ni meneja wa biashara wa kanda ya ziwa kutoka kampuni ya bia ya Serengeti  Bw. Octavian Migire, na Katibu wa Chama cha soka mkoani Kigoma Bw. Mrisho Bukuku, Bonanza hilo limedhaminiwa na kampuni ya bia ya Serengeti kupitia bia yake ya Serengeti Premium Lager. Timu za mashabiki zilizoshiriki bonanza hilo ni Chelsea, Liverpool, Real Madrid, Barcelona, Bayern Munich, AC Milan.

Nahodha wa timu ya mashabiki wa Manchester United mkoani Kigoma akipokea kombe la ushindi wa pili na kitita cha fedha taslimu laki mbili kutoka kwa meneja wa biashara kanda ya ziwa kutoka kampuni ya bia ya Serengeti  Bw. Octavian Migire anayeshuhudia ni Mkurugenzi wa Utafiti wa Clouds Media Group Bw. Ruge Mutahaba baada ya kuibuka washindi wa pili katika bonanza la Serengeti Fiesta Soccer Bonanza lililofanyika siku ya ijumaa jioni katika uwanja wa Kawawa uliopo Ujiji,  , na Katibu wa Chama cha soka mkoani Kigoma Bw. Mrisho Bukuku (mwenye Kaunda suti), Bonanza hilo limedhaminiwa na kampuni ya bia ya Serengeti kupitia bia yake ya Serengeti Premium Lager. Timu za mashabiki zilizoshiriki bonanza hilo ni Chelsea, Liverpool, Real Madrid, Barcelona, Bayern Munich, AC Milan.

No comments:

Post a Comment