Search This Blog

Friday, July 19, 2013

TITO VILANOVA ARUDIWA TENA NA KANSA - BARCELONA WAITA MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI HUKU TAARIFA ZIKISEMA KOCHA HUYO AMEJIUZULU

Barcelona wameita mkutano wa waandishi wa habari kwa haraka, huku kocha Tito Vilanova akitegemewa kujiuzulu kutokana kudhoofu kwa afya yake tena.

Raisi wa Barcelona Sandro Rosell na mkurugenzi wa soka Andoni Zubizarreta watakutana na waandishi jioni hii, wakatalunya wametangaza kupitia mtandao wao.

Vilanova alirithi mikoba ya Pep Guardiola mwaka jana lakini utawala wake umefunikwa na wingu la matatizo ya afya yake.

Kocha huyo wa zamani wa Barcelona B alikosa sehemu ya msimu uliopita baada ya kwenda jijini New York kutibiwa kansa.

Aligundulika kuwa na kansa mnamo November 2011.

Vilanova anaaminika kuwa ugonjwa wa kansa umemrudia tena, huku akiwa na jukumu la kuiongoza moja ya klabu kubwa duniani.


1 comment:

  1. Andreas Villa Boas ana nafasi kubwa sana ya kumrithi

    ReplyDelete