Search This Blog

Thursday, July 4, 2013

PICHA YA SIKU: BARCELONA WAMUONDOA THIAGO ALCANTARA KWENYE TANGAZO LA JEZI NA TOUR KWENYE AKAUNTI YAO YA INSTAGRAM


Klabu ya Barcelona imemkata mchezaji wao Thiago Alcantara anayewania na Manchester United kwenye tangazo la kuitangaza tour yao pamoja na jezi mpya waliloweka kwenye akaunti yao rasmi ya mtandao wa kijamii wa Instagram. Thiago kwa muda mrefu sasa ametajwa kutaka kuondoka kwenye klabu hiyo huku vyombo vya habari vikiripoti kwamba ndani ya wiki hii mchezaji huyo atakuwa ameshajiunga na United chini ya David Moyes. FC Barcelona na United zote hazijakanusha wala kukubali taarifa hizi - ila kwa kitendo cha Barca kukata sura ya Thiago kwenye picha ambayo mwanzoni alikuwepo kimezidi kuzipa nguvu tetesi za mchezaji kuhamia Man United. Lakini hizi zote ni tetesi na hakuna kilichothibitishwa.
Picha ya juu inaonyesha ilivyokuwa mwanzo Thiago akiwepo - wakati hii ya chini ni ya leo ikiwa sura ya Thiago Alcantara haijakwatwa.

2 comments:

  1. apana mi ninacho fikiria nahic ndo atakua mrithi wa xavi kutokana na umri wa mkongwe huyo kuwa mkubwa so nahisi ni tetesi tuuuu na thiago hana safari bt lets wait n c

    ReplyDelete
  2. Me naona thiago aje 2 man utd 2wakomeshe league kuu england

    ReplyDelete