Search This Blog

Friday, July 5, 2013

NICOLAS ANELKA ARUDI TENA ENGLAND - ASAJILIWA NA WEST BROM NA KUWEKA REKODI YA KUCHEZEA KLABU 6 ZA LIGI KUU YA ENGLAND


West Brom wamethibitisha kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Ufaransa Nicolas Anelka.

Mshambuliaji huyo mwenye miaka 34, ambaye alikuwa huru, amesaini mkataba wa kuanzia wa mwaka mmoja wa kuichezea klabu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya England.

Klabu hiyo imethibitisha kupitia akaunti yake ya Twitter: 'Albion leo usiku imekamilisha usajili wa @anelkaofficiel kwa mkataba wa mwaka mmoja, huku kukiwa na hivyo.'

Kocha wa Baggies Steve Clarke, ambaye alishafanya kazi na Anelka kwa muda mfupi ndani ya klabu ya Anelka amefurahia usajili huo.
'Tulikuwa tunakosa nguvu ya ziada kwenye ushambuliaji kutoka mwaka jana, tunajaribu kuweka hilo sawa - na kwa kuanzia kwa usajili wa  Nicolas,' aliuambia mtandklabu hiyo wba.co.uk.

Anelka sasa anazidi kujiandikia rekodi ya kuwa mchezaji aliyevicheza vilabu vingi kwenye ligi kuu ya England baada ya kuitumikia Arsena, Chelsea, Liverpool, Manchester City, Bolton


VILABU VYOTE ALIVYOCHEZEA ANELKA
Senior career*
YearsTeamApps(Gls)
1996–1997Paris Saint-Germain10(1)
1997–1999Arsenal65(23)
1999–2000Real Madrid19(2)
2000–2002Paris Saint-Germain39(10)
2001–2002→ Liverpool (loan)20(4)
2002–2005Manchester City89(37)
2005–2006Fenerbahçe39(14)
2006–2008Bolton Wanderers53(21)
2008–2012Chelsea125(38)
2012–2013Shanghai Shenhua22(3)
2013→ Juventus (loan)3(0)
2013–West Bromwich Albion0(0

No comments:

Post a Comment