Search This Blog

Tuesday, July 30, 2013

MICHEZO NA UTU - CRISTIANO RONALDO ASAFIRI MPAKA GALICIA KWENDA KUTOA DAMU KWA MAJERUHI WA AJALI YA TENI

ronaldo-blood
Kwa mujibu wa ripoti katika vyombo vya habari za Spain - Cristiano Ronaldo alisafiri kutoka jijini Madrid kwenda mpaka ilipotokea ajali ya treni huko Galicia na kwenda kuchangia damu kwa majeruhi wa ajali ya hiyo ya treni iliyotokea karibu na kaskazini mashariki mwa Santiago de Compostela.

Inasemekana kulikuwepo na majeruhi zaidi ya 160 huku watu wengine 0 wakifariki dunia. 

Pamoja na kuripotiwa kufanya kitendo hicho, nyota huyo wa Real Madrid alitumia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter kutoa pole kwa wahanga wa ajali hiyo

Aliandika 
“Ni huzuni mkubwa kwamba nimesikia habari za ajali ya treni nchini Spain. #animogalicia”

“Ninaungana na ndugu jamaa na marafiki wa wahanga wa ajali na nawaomba watu wengine mkasaidie majeruhi wa ajali hiyo. #animogalicia”
          

No comments:

Post a Comment