Search This Blog

Saturday, July 6, 2013

MARIO GOTZE, GOMEZ NA KIRCHHOFF WAPIGWA FAINI NA BAYERN MUNICH KWA KUVAA MAVAZI YA NIKE



Bayern Munich imewapiga faini Mario Gomez, Mario Gotze na Jan Kirchhoff kwa kuvaa mavazi ya Nike wakati wa matukio rasmi ya FC Bayern - hivyo kuleta mtafaruku na wadhamini wa klabu Adidas, amesema afisa wa habari wa klabu hiyo Markus Horwick.

Klabu hiyo ya Bundesliga ina sheria ya kuwalazimisha wachezaji wake kuvaa mavazi ya Adidas katika shughuli rasmi za klabu hiyo - ni viatu pekee ambavyo wanaruhusiwa kuvaa vyovyote.

Ingawa, wote wawili Gotze na Kirchhoff walipokuwa wakitambulishwa kujiunga na klabu hiyo walionekana wakiwa wamevaa mavazi ya fulana zenye logo za Nike - ambao ni wapinzani wakuu wa kibiashara na Adidas.
Bayern tayari wameomba samahani kwa kampuni ya Adidas, lakini wakiwa wamefanya hivyo muda mchache baadae Mario Gomez akapigwa picha akiwa amevaakofia yenye logo ya Nike kwenye uwanja wa mazoezi.

Matokeo yake mabingwa wa ulaya wakaamua kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya wachezaji wote watatu kwa kuwapiga faini, ambazo zitaenda kwenye kusaidia wahanga wa mafuriko nchini Ujermani.
Wachezaji wote wamekubali faini zao, lakini hakitajwa kiasi cha faini hizo.

No comments:

Post a Comment