Search This Blog

Thursday, July 4, 2013

KIBADENI KOCHA BORA, YONDANI MWANASOKA BORA, NA YANGA NDIO TIMU YENYE NIDHAMU - TUZO ZA VODACOM PREMIER LEAGUE



Beki wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga kwenye klabu ya Yanga, Kevin Patrick Yondan amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2012/2013 na kuzawadiwa donge nono la Sh. Milioni 5. Yondani ambaye alihamia Yanga akitokea Simba amechaguliwa kuwa mwanasoka bora VPL baada ya kuwa na msimu mzuri na klabu yake ya Yanga ambayo ilitwaa ubingwa huo huku akiruhusu mabao machache kuliko timu nyinginezo.
Vodacom pia ilitoa tuzo kwa kocha na bora na wachezaji wengine waliofanya vizuri msimu uliopita na tuzo zilikuwa kama zifuatazo

Top Scorer- Kipre Tchetche Azam (5m)
Best Player- Kevin Yondani (5m)
Best Coach Abdallah Kibadeni Kagera (7.5m),
Best Goalkeeper- David Burhani Prisons (5m)
Mchezaji mwenye nidhamu- Fulli Maganga JKT Ruvu (5m)
Team yenye nidhamu- Yanga (15m)

12 comments:

  1. Yondani kawa bora kwa kigezo kipi? mbali na Kiple Cheahe kuwa mfungaji bora bado alistahili kuwa mchezaji bora. Yanga wamekuwa na hidhamu kwa sababu gani?

    ReplyDelete
  2. Nadhani wangempa Nyonzima kwasababu alisaidia Yanga kuchukua ubingwa pia alitoa past nyingi za magoli na akafunga Magoli tena Kwenye mechi ngumu. Tuache ushabiki wa kipuzi.....

    ReplyDelete
  3. tuzo za kisanii hizi, yanga wamepewa tuzo ya timu yenye nidhamu kivipi??? wanaweza kuweka vigezo vilivyo realistic and justifiable???

    ReplyDelete
  4. figo wa box 2 boyzJuly 4, 2013 at 3:58 PM

    mmh hii timu yenye nidhamu c ndo inaomgoza kwa kupiga waamuzi lakini?kwl soka la bongo simba na yanga.....

    ReplyDelete
  5. KWELI SOKA LA TANZANIA MAJANGA!!!HUYO KIPA BORA WAMEFUATA VIGEZO GANI

    ReplyDelete
  6. Jaman hv kuna data zozote ambazo wametumia kuchagua hizi madudu yao! Ok yanga nidhamu bora!walipata kadi red ngapi yellow ngapi? Kipa bora kafungwa goli ngapi? Kocha bora mzalendo au kocha bora kwa kutwaa ubingwa au kuifanya timu iwe bora?
    Mm naamini soka la bongo ni mambo ya uamuz wa watu tu wachache tu! Kwan wanajua hakuna wa kuuliza!!

    ReplyDelete
  7. Kwa uelewa wangu kocha bora ni lazima afanye kitu cha maana katika timu ikiwezekana kuchukua kombe au kushika nafasi tatu za juu lakini hapa bongo hilo halionekani!!
    Pia kipa bora ni yule aliyeruhusu lango lake kufungwa magoli machache lakini huyo wa prison cjui katoka wapi au ndo mambo ya bora tuzo c tuzo bora!!

    ReplyDelete
  8. Kwa upande wa makocha inaonekana makocha wa kigeni hawana chao haiwezekani timu iliyoshika nafasi ya kwanza mpaka ya tatu makocha wao wakose tuzo ya kocha bora!!

    ReplyDelete
  9. zote ziko sawa isipokua kibadeni hakustahili

    ReplyDelete
  10. labda uzalendo maana wale wengine(SPUTANZA) walimpa mecky maxime ukocha bora.Halafu waqkampa Sure Boy mchezaji bora chipukizi akiwa na umri wa miaka 23 na huo ulikuwa msimu wake wa nne anacheza ligi kuu akiwa first eleven tunadanganywa bado anachipukia.Tusubiri madudu mengine zaidi Tuzo za TASWA

    ReplyDelete
  11. Wamebugi hao yaani nilishangaa hata tuzo za TASWA kocha bora kapatikana kisa kazifunga yanga na simba wakati kwenye ligi kuna timu 14 asa najiuliza huyu kapatikana vipi? lakini sikushangaa sana baada ya kusikia amepatikana kwa kupigiwa kura na makocha wenzake pamoja na manahodha kwa hiyo kigezo ni kura wala si data
    Lakini mpaka kwenye tuzo hizi za vodacom bado data hazijatumika kumpata kocha bora!!! Hapa nadhani makocha wa kigeni wasahau kuchukua tuzo

    ReplyDelete